Home

  • Hivi Ndivyo Unavyopaswa Kuwa Mwanasayansi Wa Maisha Yako.

    Rafiki yangu mpendwa wanasayansi huwa wanafanya majaribio mbalimbali,wanakusanya taarifa, wanafikia hitimisho na kisha kuondoka na kile walichogundua.

    Wanasayansi wanapofanya majaribio hawaanzi wakiwa na jibu fulani, hivyo wanakuwa tayari kupokea jibu lolote na kujifunza.

    Rafiki, hivyo ndivyo unavyopaswa kuwa kwenye unachofanya. Iwe ni kazi au biashara, kila wakati, jaribu vitu vya tofauti, angalia matokeo unayopata kisha jifunze na boresha zaidi.

    Majaribio hayo hayapaswi kuwa na mwisho hata kama umefanikiwa kiasi gani. Endeleza majaribio hayo kwenye kila fursa unayopata ama wazo lolote lile na kwa kufanya hivyo unapaswa kupima na vigezo 5 vya majaribio kama ambavyo tumejifunza kwenye somo la jana.

    Chukua hatua, wewe angalia kile ambacho umeshazoea kufanya na jiulize kwamba vipi kama ningekifanya hivi. Hata kama inaonekana ni njia ya ajabu, usijipe majibu mwenyewe, fanya jaribio na utajifunza mengi ya kukuwezesha kujiboresha zaidi.

    mwandishi wako,

    Maureen Kemei,

    kemeimaureen7@gmail.com.

    uamshobinafsi.com

  • Sifa 5 Za Jaribio Sahihi Kufanya.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini ili ufanye jaribio, lazima uwe na vigezo unavyoviangalia.

    Kwenye kitabu cha skip the line mwandishi anatushirikisha vigezo vitano vya kuzingatia unapofanya jaribio.

    Moja iwe rahisi kuanza,kwa kuwa utafanya majaribio mengi,basi la kwanza lazima liwe rahisi kufanya. Uweze kuanzia pale ulipo sasa bila kuhitaji kitu chochote cha nyongeza ambacho huna. Hupaswi kutumia muda nyingine kusubiri ili kuanza jaribio, linapaswa kuwa rahisi na uweze kuanza mara moja, ili uone matokeo yake na usonge mbele.

    Mbili hatari iwe ndogo na ndani ya uwezo wako. Hatari iliyopo kwenye jaribio unalofanya uwe ndogo na ndani ya uwezo wako kuikabili. Usifanye jaribio ambalo lina hatari kubwa kwako kuweza kupoteza kila kitu kinaweza kudhurika kwa namna fulani. Jua kabisa hatari ya jaribio unalofanya ni ipi,kama litashindwa kabisa, hasara utakayoipata ni ipi. Kisha ona kama ni kitu kipo ndani ya uwezo wako ufanye.

    Tatu faida unayoweza kupatikana iwe kubwa. Kwa kuwa majaribio utakayoifanya ni mengi na mengi utaishia njiani unapaswa kuchagua jaribio kwa kigezo kwamba kama litafanikiwa basi faida linapaswa kuwa kubwa sana kufidia majaribu mengine ambayo hayatafanikiwa. Na hata kama siyo faida ya kifedha,basi jaribio liweze kuleta mapinduzi makubwa kwenye tasnia husika.

    Nne iwe ni kitu ambacho hakijawahi kufanywa. Jaribio linapaswa kuwa kitu kipya ambacho hakijawahi kufanywa kabisa na hivyo hujui matokeo gani yatakayopatikana. Kama wazo lilishafanyika huwezi tena kusema ni jaribio, maana njia ya kufanya tayari inajulikana.

    Tano ni kuwepo na kitu cha kujifunza. Katika kila jaribio unalofanya,haijalishi ni matokeo gani utapata, basi uwe na kitu ambacho utajifunza. Hata kama jaribio litashindwa kuleta matokeo uliyotaka, angalau ujifunze kitu ambacho kitakusaidia kwenye majaribio mengine. Katika majaribio unayofanya, hakuna kushindwa, unapata unachotaka au unajifunza kitu kipya.

    Rafiki, kwa kuzingatia sifa hizi tano,utaweza kufanya majaribio yenye tija kwako na kama utayafanya mengi, lazima utakutana na jaribio litakaloleta matokeo mazuri na ukafanikiwa.

    Na kama Thomas Edison alipoulizwa kuhusu kushindwa mara nyingi katika kutengeneza taa zaa umeme alijibu hakushindwa, bali alijua njia ambazo hazifanyi kazi.

    Chukua hatua, rafiki kwa kila jaribio ujifunze ili unapoenda kwenye jaribio jingine uweze kulifanya kwa ubora zaidi kuliko jaribio lililopita.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Kuwa Bora Kwa Asilimia 1 Kila Siku.

    Rafiki yangu mpendwa sheria ya asilimia moja kila siku ni kukazana kuwa bora zaidi kila siku kwa asilimia moja kuliko ulivyokuwa siku iliyopita.

    Kwa kila siku mpya unayoianza, pambana kujiboresha kwa asilimia moja zaidi ya siku iliyopita kwenye kile unachofanya.

    Unaweza kuiona asilimia moja ni ndogo na kuidharau, ila hujajua nguvu yake. Kama utaifanyia kazi sheria hiyo kwa mwaka mzima, ukakazana kuwa bora kwa asilimia 1 zaidi kila siku kwa siku 365, unadhani mwisho wa mwaka utakuwa bora kwa asilimia ngapi?

    Kwa hesabu ya haraka utasema unakuwa bora kwa asilimia 365, lakini hiyo siyo kweli. Kwa kuwa bora kwa asilimia moja zaidi kila siku, kwa siku 365 unakuwa bora kwa asilimia 3,800.

    Ndiyo, yaani unakuwa bora mara 38 ya ulivyoanza na hapo ni kwa mwaka mmoja tu. Kinachofanya ubora wako uwe mkubwa hivyo ni nguvu la ongezeko la mkusanyiko compounding.

    Siku ya kwanza unakuwa bora asilimia 1, siku ya pili unakuwa bora kwa asilimia 1 zaidi ya siku ya kwanza.

    Siku ya tatu unakuwa bora kwa asilimia moja zaidi ya siku ya pili. Kwa hiyo ubora wako unakua kwa mkusanyiko na siyo kwa mstari.

    Chukua hatua, kwa kukazana kuwa bora kwa asilimia moja zaidi kuliko ulivyokuwa siku iliyopita, unajikuta ukiwa umepiga hatua kubwa ndani ya mwaka mmoja kuliko ambazo wengine wanapiga kwa miaka 10.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

    uamshobinafsi.com

  • Dhibiti Kile Kinachoingia Kwenye Akili Yako.

    Rafiki yangu mpendwa tunaishi kwenye zama ya mafuriko ya taarifa na maarifa, tuna mengi yanayopigania kupata umakini wetu kuliko muda tulionao wa kuhangaika na mambo yote hayo.

    Watu wengi wamekuwa wakijidanganya kwa kukimbizana na maarifa zote ili wasipitwe, lakini kwa kumezwa na taarifa hizo, wanakosa muda wa kufanya mambo mengine muhimu.

    Sina uhakika kama itakufaa, lakini usikubali hili litokee kwako, badala ya kuhangaika na kila aina ya taarifa na maarifa yanayosukumwa kuja kwako, dhibiti ni aina gani ya maarifa zikufikie na kwa muda gani.

    Fikiria jinsi ambavyo huwa unajisikia unapoamka asubuhi na mapema, kabla siku hazijaanza kuingia na hujaanza kuzurura mitandaoni. Unakuwa na utulivu mkubwa sana ndani yako, unaweza kufanya makubwa na mazuri.

    Chukua hatua, rafiki sasa tengeneza hali kama hizo kwenye maisha yako, tenga muda wa kuwa mbali na maarifa na taarifa na kuweza kufikiri kwa kina na kufanya kazi ambayo inahitaji utulivu wako.

    Muda huo kaa mbali kabisa na simu yako na hata watu wengine, ili uepukane na usumbufu utakaoathiri kile unachofanya.

    mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com

  • Njia 2 Za Kuongeza Kujikubali Wewe Mwenyewe.

    Karibu rafiki nini tunachoweza kufanya na maisha yetu yanatokana na historia na mtazamo wa maisha yetu.

    Unakuta mtu anafanya makubwa na anapata matokeo lakini hajikubali. Kama anaweza kufanya zaidi ya hapo, anaanza kuogopa na kujidharau kupitia ujumbe hasi ambao umekuwa unaupokea mara kwa mara siku za nyuma.

    Njia ya kutoka kwenye hali ya kutokujiamini, kutokujithamini na kutokujikubali ni kwa kujiambia maneno chanya mara kwa mara bila kuacha.

    Kitu cha pili ni kusanya ushahidi wa zile kauli chanya unazojiambia kupitia matokeo unayopata hata kama ni machache na endelea kupiga hatua.

    Hata kama matokeo yamekuja tofauti na ulivyotegemea, badala ya kuhalalisha kwamba mimi siwezi kufanya vizuri na watu wengine wanathibitisha hilo kukudhibitishia kuwa huwezi, unapaswa kujiambia kauli chanya ya kuboresha makosa kama vile wakati mwingine nitafanya hivi na vile.

    Chukua hatua; rafiki tunapaswa kufanya tuwezavyo kwa chochote tunachofanya na malengo yetu. Kwa kujithamini,kujiamini na kujikubali.

    Rafiki kwa kila hatua unayotaka na kufanya jiambie kauli chanya.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei .

    kemeimaureen7@gmail.com.

    uamshobinafsi.com.

  • Hatua 3 Muhimu Za Kukuwezesha Kutengeneza Maana Ya Maisha Yako.

    Rafiki yangu mpendwa kutengeneza maana kwenye maisha ni matokeo ya kutengeneza utaratibu kwenye ufahamu wako.

    Ni kuyaelekeza yale yote unayofanya katika kuzalisha hali ambayo inayafanya maisha yako kuwa bora zaidi.

    Hatua la kwanza ni unapaswa kuwa na kusudi la maisha yako, unapaswa kuwa na kitu ambacho kinakusuma kuweka juhudi zaidi kwenye yale unayofanya kwenye maisha yako.

    Kusudi lako la maisha ndiyo linalokusuma kuweka umakini wako kwenye yale unayoyafanya na hata kujituma zaidi pale unapojisikia kukataa tamaa. Kusudi la maisha ndilo linalokuwezesha kuvuka vikwazo na magumu mbalimbali tunayokutana nayo.

    Mbili ni kuwa na malengo ambayo yanakufikisha kwenye kusudi la maisha yako. Kusudi lako halitafikiwa kama ajali, lazima ukae chini uweke malengo na mipango itakayokuwezesha kufikia kusudi hilo.

    Malengo yako ndiyo yanayoamua wapi uweke umakini na jinsi gani utumie nguvu za ufahamu wako. Bila ya malengo utatawanya vibaya nguvu zako za ufahamu, utachoka huku ukiwa hakuna kubwa ulilofanya. Malengo ndiyo yanayotuweka kwenye mstari wa kulifikia kusudi la maisha yetu.

    Tatu ni kuwa na maelewano kati ya kusudi na malengo, hili ndiyo muhimu sana kwa sababu bila ya maelewano mazuri baina ya kusudi lako na malengo unayoweka, hutaweza kupiga hatua. Lazima kila unachofanya kiwe kinachangia kwenye kufikia kusudi lako, na fikra zako ziwe kwenye unachofanya.

    Rafiki, kila unachofanya lazima uweze kukielezea kinachangiaje kwenye malengo na kusudi la maisha yako.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

    uamshobinafsi.com.

  • Kwa Nini Hatupendi Kubadilika.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini yapo mambo ambayo tumekuwa tunajidandanya sana kwenye mafanikio, na haya yamekuwa yanachochea matatizo mengi tunayokutana nayo kwenye maisha.

    Mambo yanayochangia tusibadilike ni kama yafuatayo;

    Kwanza; tunajikadiria zaidi kwenye mchango wetu kwa mafanikio tunayofanya. Tunafikiria bila sisi mafanikio yasingepatikana, huku ni kujidanganya.

    Pili ; tunachukua sifa ambazo hatustahili kuchukua, kazi wamefanya wengine lakini wewe kama kiongozi ndiye unayetaka upewe sifa.

    Tatu; Huwa tunajiona tuna ujuzi WA juu kuliko wale wanaokuzunguka.

    Nne; huwa tunapuuza muda na gharama ambazo tumeshapoteza kwenye miradi ambayo haizalishi.

    Tano; kukuza matarajio ya mafanikio ya mradi, kuwa na mategemeo makubwa kuliko uhalisia.

    Rafiki, uongo huu unatokana na mafanikio tuliyopata uko nyuma. Tunapopata mafanikio kidogo, huwa tunajiamini zaidi ya uhalisia.

    Kujiamini huku kulikopitiliza ndiyo kunawaingiza wengi kwenye matatizo na kuwazuia kufanikiwa zaidi.

    Mwandishi na rafiki yako,

    Maure Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

    uamshobinafsi.com.

  • Umuhimu Wa Kujitofautisha Na Wengine

    Rafiki yangu mpendwa ili kufikia mafanikio makubwa na kutengeneza ubobezi wako, unahitaji kujitofautisha na wengine ambao wanafanya kile unachofanya wewe.

    Lazima kuwe na kitu ambacho watu wanakipata kwako na hawawezi kukipata kwa mtu mwingine yeyote.

    Na hili ni rahisi kujua na kutumia kama utajitafakari wewe binafsi na kuangalia maeneo yote ya maisha yako.

    Angalia uzoefu wako wa nyuma, angalia vipaji ulivyonavyo kisha ona unawezaje kuvitumia kwenye kile eneo unalojenga ubobezi na kuweza kujitofautisha na wengine wanaofanya kile unachofanya.

    Hakuna ubobezi kama hakuna kinachokutofautisha na wengine. Lazima kuwe na sababu kubwa ya watu kuja kwako.

    Kabla hujafanya maamuzi, lazima watu wajue kuna kitu wanapata kwako ambacho hawawezi kukipata kwa wengine.

    Habari njema ni kwamba ni rahisi sana kujitofautisha na wengine kama utaamua kuwa wewe. Kama utaacha kuiga na kujilinganisha na wengine, na kuchagua kuwa wewe, kwa kuweka utu wako kwenye kile unachofanya, basi utakuwa tofauti kabisa na wengine.

    Kitu kimoja zaidi rafiki ni kuwa hakuna mtu anayefanana na wewe kwa kila kitu hapa duniani. Hivyo ukichagua kuwa wewe, utajitofautisha na wengine wote.

    Chukua hatua, ili kufanya makubwa kwenye maisha yetu, tunapaswa kuanza sasa kukataa kuiga wengine na kuamua kuwa sisi na tutaweza kujitofautisha na wengine na kuweza kufanya makubwa.

    Mwandishi na rafiki yako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com

  • Njia 6 Za Kupata Furaha.

    Rafiki yangu mpendwa, sina uhakika kama itakufaa, lakini kuna njia sita nzuri kabisa unazoweza kufanya ili kuwa na furaha siku zote za maisha yako.

    Kwanza. Usiwe na kazi, kuwa na kile unachopenda kufanya. Furaha ni matokeo ya kufanya kile unachopenda kufanya.

    Hivyo, unapaswa kupenda unachofanyana hapo hutafanya kazi kabisa. Kama unachofanya unakiona ni kazi tu, basi tayari unakosea.

    Pili. Furahia kushindwa kwako. Hakuna mtu aliyewahi kufanikiwa sana bila ya kushindwa. Hivyo unaposhindwa furahia, kwa sababu ni njia ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa.

    Tatu. Fedha siyo sawa na furaha. Lengo lako kuu kwenye kile unachofanya lisiwe fedha, bali anza kwa kupenda kile unachofanya na kutoka mchango wako kwa wengine. Na furaha unayoweza kuipata kwenye fedha ni kuwasaidia wengine.

    Nne. Shukrani inaleta furaha. Unapokuwa mtu wa kushukuru, unakuwa na furaha. Kila siku orodhesha vitu unavyoshukuru kuwa navyo kwenye maisha yako na utakuwa na maisha yenye furaha.

    Tano. Utajiri hauwezi kununua afya. Hivyo weka kipaumbele cha kwanza kwenye afya yako. Wengi wanasahau afya zao kwa kukimbizana na utajiri, halafu wakishaupata wanautumia kuboresha afya zao, huo ni ujinga. Zingatia afya yako, kula vizuri, fanya mazoezi na pata muda wa kupumzika.

    Sita. Wakati sahihi kwako kubadili kazi au biashara ni pale kila unapoamka asubuhi hujiskii kabisa kwenda kwenye kazi au biashara yako. Unapoanza kujiona unafanya kazi, hapo umeshapoteza.

    Kuchukua hatua, rafiki kumbuka ili kufanikiwa hupaswi kufanya kazi, basi unapaswa kufanya kile unachopenda.

    Rafiki na mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

    uamshobinafsi.com.

  • Jinsi Ya Kuishi Wito Wako.

    Rafiki yangu mpendwa kila mtu ana wito fulani ndani yake, asili inayomvuta zaidi kufanya zaidi vitu vya aina fulani.

    Sina uhakika kama itakufaa, lakini mtu anapofanya kitu cha wito wake,anafurahia anakuwa na hamasa na hachoki,anajituma zaidi katika kukifanya.

    Wale wanaofanikiwa sana ni wale wanaojua wito wa maisha yao na kuuishi kwa viwango vya juu sana.

    Kwa kuishi wito wako, anza kwa kuangalia vitu ambavyo ulikuwa unapenda kufanya au kufuatilia tangu ukiwa mdogo.

    Kisha ingia kuvifanya kama kazi au biashara inayokulipa, huku ukiendelea kujifunza kuhusu unachofanya na kuhusu wewe mwenyewe na kuendelea kujiboresha zaidi.

    Kwa kwenda hivyo, utajikuta umetengeneza kazi au biashara ya kipekee kwako inayowanufaisha watu na inayokulipa sana.

    Rafiki uzuri wa kuishi wito wako ni hakuna anayeweza kushindana na wewe, akakushinda, maana hapo unakuwa unaishi maisha na siyo kuyaigiza.

    Kuchukua hatua; rafiki anza kujua na kuishi wito wako ili kufanya makubwa na kufurahia maisha yako ukiwa hai hapa duniani.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

    uamshobinafsi.com.