Kupata tumaini la maisha.

Zawadi tuliyopewa sisi wanadamu siyo kuona bali kuwa na maono makubwa juu ya maisha tunayotamani kuyaishi. Lakini, ni muhimu pia kufurahia kile ulicho nacho wakati unapambana kupata kilicho kubwa zaidi.

Hapo ndipo chanzo cha tumaini kinaanza, kufurahia ulichonacho huku ukiwa makini usiridhike sana na hapo ulipo. Unapambana kufikia ndoto na maono yako makubwa.

Hiyo ni njia ya kwanza kabisa ya kuondokana na matatizo au msongo yanayoweza kukukwamisha. Kuwa na ndoto kubwa au maono makubwa yanayokuwajibisha kwelikweli. Litakufanya uwe ‘bize’ wakati wote kukimbiza ndoto yako na usumbufu wowote ule hakutakuwa na nafasi kwako.

Hatua ya kuchukua leo, kwa vile sisi binadamu tumetumwa hapa duniani kukamilisha kitu maalumu, tunahitaji kujiwekea malengo makubwa na yanayotimika.

Hii ni njia mojawapo ya kufahamu ni nini hasa tunapaswa kutimiza kabla masiku yetu hayajaisha hapa duniani. Na hapo tunapata tumaini ya kesho bora au mwisho wetu kuwa bora.

Mimi akujaliye.

Maureen Kemei.

Blog, kufikirichanya.wordpress.com

By Maureen Kemei

Author, psychologist.