-
Mambo muhimu ya kujifunza kutoka kwa mwanaharakati Desmond Tutu.
Kutoka katika kitabu cha ‘everyday ero manifesto ‘ mwandishi Robin anatushirikisha wakati alipokutana na Desmond Tutu, mwanaharakati wa Africa kusini aliyefanya kazi kwa karibu na Nelson Mandela katika kuikomboa Afrika kusini na kuponya mfumo wa ubaguzi.
Robin anasema kitendo cha kukutana na Desmond kilileta nguvu kubwa na ya kipekee ndani yake,kupitia yeye kuna mambo makubwa muhimu sana aliyojifunza.
Mambo hayo ni kama yafuatayo:
Kuwa jasiri kusimamia kile kilicho sahihi bila ya kujali nani anayekupinga ,lakini pia kuwa tayari kuwasamehe waliokuumiza kwa namna mbalimbali.
Kila binadamu hapa duniani ni muhimu bila kujali rangi, jinsia,dini au utaifa. Na kila mtu anapaswa kuchukuliwa kwa heshima uelewa na upendo.
Umuhimu wa kila mtu kuishi upekee ambao upo ndani yake,kuvunja minyororo ya ukomo ambayo tumejengewa na kuwa halisi ,kitu ambacho kina mchango mkubwa hapa duniani.
Kila mtu ni kiongozi hata kama hana madaraka. Asili huwa haipendi kuwepo kwa utupu, hivyo popote ulipo ,asili itakupa wajibu wa kuwa kiongozi Ili kujaza ombwe lililopo. Ni wajibu wako kuwa na maono na kuwahamasisha kuyaelewa na kujiunga na maono uliyonayo.
Sisi binadamu tuna nguvu kubwa ambayo tayari ipo ndani yetu ,ni wajibu wetu kuitambua na kuanza kuitumia Ili kuweza kufanya makubwa.
Mwandishi wako akupendaye sana.
Maureen Kemei.
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Hatua 10 za kuchukua Ili kuweza kuwa na utulivu wa mwili.
Kila tunachoweka kwenye miiili yetu na jinsi tunavyoitumia na kuhifadhika kwenye miili yetu,kunachangia sana kuwa na utulivu au kukosa utulivu.
Njia ya kwanza ni kujifunza kusema hapana . Rasilimali kama muda na nguvu ni rasilimali mbili ambazo tunazo kwa uhaba ,tunapaswa kuzitumia kwa umakini sana. Unaposema ndiyo kwenye vitu visivyo muhimu,unasema hapana kwenye yaliyo muhimu.
Njia ya pili ni kwenye kufanya matembezi. Tunapaswa kutenga muda ya kufanya matembezi Ili kuondokana na mkwamo. Matembezi pia ni njia bora ya kufanyia mwili mazoezi,na pia njia bora ya kutafakari kuhusu maisha kwa ujumla.
Njia ya tatu ni kuondokana na vitu ambavyo huvitumii. Tunapochukua hatua ya kupunguza vitu ambavyo tunavimiliki ,ndivyo tunavyotoa nafasi na nguvu kwenye yale ambayo ni muhimu zaidi kwenye maisha.
Njia ya nne ni kwenye kutafuta upweke. Kwa kujitenga na kukaa peke yako kwa muda itakupa nafasi ya kutafakari na kufikiri vizuri,kusali na pia kutahajudi.
Njia ya tano ni kuwa mtu. Kwa asili tunapaswa kupata muda wa kupumzika,muda wa kutafakari,muda wa kujua ukomo wa uwezo wetu na pia kuishi ndani ya ukomo huo.
Njia ya sita ni kwenye kupata usingizi wa kutosha. Usingizi ni riba tunayolipa kwa kuwa na maisha, hivyo kama hatupati usingizi wa kutosha maana yake hatulipi riba. Usingizi siyo anasa bali ni kitu muhimu sana kwetu kama tunataka kuwa wa mwili imara wenye utulivu.
Njia ya sapa ni kuwa shujaa . Maisha tunayoishi sasa imekuwa ya ubinafsi mkubwa,kila mtu anasumbuka na mambo yake na hataki kujua kuhusu nwenzake. Ili kuwa shujaa wa kweli tunapaswa kukataa ubinafsi na kuwa tayari kutoa mchango wetu kwa wengine,na pia kusimamia kilicho sahihi mara zote.
Nane ni kutafuta hobi. Ili mwili wetu upate utulivu ,hasa pale unapofanya kazi kwa muda mrefu , unapaswa kuwa na hobi. Ni kitu ambacho unapenda kukifanya na siyo tu unafanya kwa sababu unapaswa kufanya. Na pia siyo kwa sababu unafanya Ili wengine wakuone.
Tisa ni kutengeneza utaratibu wa kuiendesha siku. Ili kuondokana na kupoteza nguvu nyingi ya kuamka na kutafakari ufanye nini kwanza , unapaswa kupangilia siku yako vizuri. Kwenye kutengeneza utaratibu huo,amabayo unakuwa unaiendesha siku yako. Unapangilia ni muda gani utakuwa unalala na muda gani utaamka na utafanya nini na nini.
Tukio la mwisho. Ulimwengu huu sio makao yetu,tumo humu kwa muda mchache mno ,kifo ndio tukio la mwisho kwenye maisha ya kila mmoja wetu. Kifo ndio kitu pekee ambacho hatuwezi kukikimbia. Siku tuliyozaliwa ndiyo tulipewa adabu ya kifo.
Wanafalsafa wengi huwa wanasema kuwa lengo la falsafa ni kujifunza kufa. Na njia pekee ya kujifunza kufa ni kujifunza kuishi vizuri kila siku yetu. Kuuishi kila siku kama vile ndiyo siku ya mwisho wa uhai wetu.
Kuchukua hatua ya kufikiri kwa usahihi,kujiimarisha kiroho,kutafuta maana na uzuri wa maisha. Tunapoyaendesha maisha yetu tunapaswa kuuishi na kutunza miili yetu Ili isije tukafa mapema kabla ya kutimiza ndoto zetu.
Kuishi vizuri na kwa utulivu kutayafanya maisha yetu yawe bora na kifo chetu kuwa chema.
Mwandishi wako akupendaye sana.
Maureen Kemei
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Jinsi ya kubadilisha mfumo hasi wa kufikiri.
Kuzama kwenye mawazo ya zamani ni kama utambuzi,lakini mwishowe inashawishi hisia na tabia .Kwa kubadilisha namna unavyofikiri kuhusu mambo yaliyopita,inakupa fursa ya kusonga mbele zaidi.
Tengeneza muda wa kufikiri kuhusu yaliyopita,wakati mwingine akili zetu zinahitaji fursa ya kutatua mambo na wakati mwingine na kadri unavyojiambia kwamba hutaki kufikiria kuhusu mambo hayo,ndivyo yanavyokuja kila mara. Badala ya kun’gang’ana kufutilia mbali mawazo hayo unaweza ukajiambia nitafikiria kuhusu hayo baada ya dinner. Alafu ujipe dakika tano ya kufikiria kuhusu kitu hicho. Wakati wa kufikiri ukiisha endea na kingine au ujipe wazo jingine jipya la kufikiria.
Tengeneza mpango itakayokusaidia kufikiria kuhusu kitu kingine, kwa mfano amua kuwa unapofikiri kuhusu iyo jambo au kazi yako ambayo hukufanikiwa nacho,utabadilisha fokasi yako kwa kufikiri kuhusu mipango yako au likizo yako inayofuata. Hii inakusaidia kukabiliana na fikra hasi kabla hujaenda kulala.
Weka malengo yako ya mbeleni . Haiwezekani fikra zako mara zote ni za zamani kama unapanga za mbeleni,. Unapaswa uweke malengo ya muda mfupi na mrefu alafu uchukue hatua inayohitajika Ili kufikia malengo yako . Hii itakupa kitu cha kuangalia mbele hivyo kukuzuia kwenye kufikiria ya zamani.
Mawazo yetu siyo ya kweli kama vile tunavyofikiri . Mara zote tukikumbuka nyakati mbaya,tunaongezea na kufanya kuwa changa kubwa. Kama unafikiri kuhusu kitu ulichosema kwenye mkutano kisha ukajutia ,utaona kuwa watu walikuhukumu vibaya. Ukikumbuka mawazo hasi,jaribu mikakati hizi Ili kuweka mazoea yako vizuri.
Weka fokasi yako kwenye funzo unachopata. Kama umepitia nyakati ngumu inabidi uweke fokasi yako kwenye yale unayojifunza kutoka kwenye mazoea yako . Kubali kuwa ilifanyika na ufikirie kuhusu jinsi utakavyokuwa mtu wa tofauti uliyebadilika. Kwa sababu ya hayo,kumbuka kuwa siyo lazima iwe kitu kibaya . Labda ujifunze kuongea kwa sababu uliona kama watu wanakuona wewe ni wa chini ama unajifunza kuwa wa kuaminiwa ukitaka mahusiano ya dumu. Wakati mwingine tunajifunza kutokana na wakati mgumu unm
Mawazo yako yajengwe kwenye mantiki wala sio hisia. Kufikiria yaliyo hasi mara nyingi inasumbua sana kwa sababu utaweka fokasi kwenye jinsi unavyohisi wakati wa tukio fulani. Lakini ukijikimbusha tukio hilo kupitia mantiki masumbuko yote yatapungua. Badala ya kufikiria kuhusu yaliyopita ulivyohisi ulipoenda mazishi kumbuka yote kuhusu tukio hilo; pahali ulipoketi ,nini ulijifunza ,nani alikuwepo hapo . Unapofikiria kutoa hisia za mahali hapo haitakusumbua sana.
Kuwa na matazamo wa tofauti kuhusu hali. Ukiweza kutafakari yaliyopita. Chunguza njia zingine zinazofanana ,unatawala jinsi unapokumbuka habari iyo . Habari iyo inaweza ikasambazwa mara nyingi na bado ikawa kweli . Kama ulivyosasa yanastua unaweza ukajaribu njia nyingine.
Tunapaswa kuepuka kufikiria kuhusu mambo yaliyopita na mara nyingi mawazo yetu yawe kwenye wakati uliopo . Tukifanya hivyo tutaweza kupunguza magonjwa mengi yanatokana na kufikiria magumu tuliyopitia, jinsi tulivyoumizwa na mengineyo.
Mwandishi wako akupendaye sana.
Maureen Kemei.
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Jinsi ya kujizoeza kuwa na nidhamu binafsi.
Nidhamu binafsi sio kitu ambacho unasema unayo au huna. Ni kitu ambacho kila mmoja wetu anaweza awe nacho na kuongoza. Au kuamua kutokuwa nacho na kuipuuza kabisa. Kusema hapana kwa sahani ya chipsi ama cookies inahitaji uwe na nidhamu ya kiasi.
Kama vile kwa kufanya mazoezi na kama hutaki kuepuka makosa hizi ambazo zinakurudisha nyuma inahitaji msimamo thabiti na bidii .
Yafuatayo ni mambo muhimu ya kuzingatia inapokuja kwenye kuwa na nidhamu ya kiasi.
Kujifunza kuvumilia magumu (practice tolerating discomfort) Kama unahisi upweke na unajaribiwa kuchati na ex wako ambaye siye mtu mzuri kwako. Au una uteja wa vyakula ambavyo zinaharibu afya yako. Unapaswa ujifunze uvumilie magumu ya kukosa haya yote. Ingawa watu saa zingine wanajifariji na kusema wakikubali au kufanya kitu hiki itawasaidia. Tafiti zinaonyesha tofauti,kuwa kila mara unapokubali kutovumilia magumu unapunguza uwezo wa kuwa na nidhamu ya kiasi.
Kuwa chanya kwenye maongezi Yako. (Use positive self-talk) kiuhalisia unapojitamkia kauli chanya au uchanya kila mara inakusaidia uepuke majaribu wakati wa udhaifu wako. Kujitamkia kauli kama ” Naweza fanya hiki”ama ‘ninafanyia kazi malengo yangu’ Kujitamkia hivyo inakusaidia kukaa kwenye mchakato.
Fikiria kuhusu malengo yako. (Keep your goals in mind). Kuweka focasi kwenye umuhimu wa malengo yako inapunguza majaribu. Hivyo ukiweka focasi yako kwenye kutimiza malengo na mipango yako kila siku,wiki ,mwezi na mwaka , inakusaidia sana kwenye kujenga nidhamu binafsi.
Jisukume mwenyewe ( impose restrictions on yourself). Kama unajua unaweza ukatumia fedha nyingi ukiwa unatembea na marafiki , amua kutembea na fedha zako chache . Chukua hatua ambazo zitakuwa ni vigumu kwako kushawishika kuingia kwenye majaribu haraka.
Tengeneza sababu za kwa nini hutaki kurudia makosa yaleyale. ( Create a list of all the reasons why you don’t want to repeat your mistakes). Tengeneza orodha yako na utembee nayo,unapojaribiwa kurudia kosa lako la awali . Soma kwa sauti tena orodha yako ,kwa kujizoeza hivyo kunaongeza ushawishi wako wa kukataa kurudia makosa hayo hayo kila mara. Kwa mfano, tengeneza orodha ya sababu yote ya wewe kutembea baada ya kula,unapojaribiwa kukaaa chini na kuangalia Tv badala ya kufanya mazoezi,soma orodha yako na itakuongezea hamasa yako ya kusonga mbele.
Kujenga nidhamu binafsi inaanzia kwenye kuwa na shauku kubwa ya kukua ,kujenga shauku na kuhakikisha upo juu kila wakati. Ili usirudishwe nyuma na maneno ya watu au kukatishwa tamaa.
Mwandishi wako akupendaye sana.
Maureen Kemei.
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Tatizo linalotokana na kuogopa upweke.
Mara kwa mara tunafungwa na majukumu pia na mahusiano yetu ya kila siku. Saa zingine yanakuwa mzigo kwetu kama hatutaaja au kuamua kutenga muda wa kuwa peke yako na kuamua kujiimarisha zaidi. Kwa bahati mbaya sana,umuhimu au uzuri wa kuwa peke yako mara nyingi zinaepukwa .
Watafiti wengi wanasema upweke wa kutenga muda na kuwa peke yako,una umuhimu mkubwa ambao sanasana wale wanaaogopa kutenga muda wa kuwa peke yao wanaiogopa.
Wastani wa upweke yaani muda wa kuwa pekee una manufaa makubwa sana kwa watoto. Utafiti uliofanywa mwaka wa 1997 ” the emergence of solitude as a constructive domain of experience in early adolescence.” Ilidokeza kwamba wanafunzi watano hadi watisa ,ambao wanatumia muda mwingi wa wastani peke yao wana uwezekano mdogo sana wa kuhusiana na tabia zisizofaa.
Watoto hao pia wanauwezo mdogo sana wa kupatwa na msongo wa mawazo, pia wana uwezo mkubwa wa kufaulu darasani.
Upweke ofisini unaongeza umakini. Ingawa ofisi nyingi inafanyiwa kwenye eneo la watu wengi. Tafiti wa mwaka wa 2000 ambao unaitwa “cognitive stimulations in brainstorming.” Iligundulika kwamba watu wengi wanaweza kufanya vizuri zaidi wakiwa peke yao. Kupata matokeo mazuri inahusishwa na kutenga muda wa kuwa peke yako.
Kuwa peke yako inaongeza uwezekano wa kuwa na huruma kwa wengine.Kwa kadri watu wanaotumia muda mwingi peke yao,wanakuwa na uwezo mkubwa wa kuonyesha huruma kwa wengine. Kama unatumia muda wako mwingi kuzurura mtandaoni na kuongea sana ,una uwezekano mkubwa wa kushikwa na we’vs them’ ‘mentality’ ambao unaleta tabia ya kutokuwa na roho ya huruma kwa wenzako.
Kwa kutumia muda mwingi kuwa peke yako unaongeza ubunifu. Wengi waliofanikiwa hasa kwenye usanii na uimbaji wao hupenda kutumia muda mwingi kuwa peke yao,husaidia kuwa wabunifu zaidi. Tafiti nyingi zinashauri kutenga muda wa kuwa peke yako inamaana unaongeza ubunifu.
Kuwa peke yako unaongeza uwezekano wa kuwa na afya ya akili. Ingawa kuna msisitizo wa umuhimu wa kushirikiana na wengine, ushahidi unashauri kuwa ,kutenga muda wa kukaa peke yako unastawisha mtu na kufanya awe imara kiakili. Kuweza kuwa peke yako husaidia mtu kuwa wa furaha, kutosheka na pia kuongeza uwezo wa kutawala usongo wa mawazo. Wanaofurahia muda wa kuwa peke yao wanapata asilimia ndogo ya sonona.
Muda wa kuwa peke yako unakusaidia ujitafakari na kukusaidia urejelee utu wako na ujikubali jinsi ulivyo. Pia unakutoa kwenye kufuata mkumbo inaleta fursa ya kujiboresha na kujiongeza . Utafiti unaonyesha kwamba kutenga muda huo wa kuwa peke yako kwa asili inakusaidia uwe upya tena kwa sababu ya mapumziko mazuri ya utulivu.
Mwandishi wako akupendaye sana.
Maureen Kemei.
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Jinsi ya kujichumbia wewe mwenyewe.
Kupanga tarehe yako solo.

1.2.2023. Kifunguo pekee cha kujitengenezea muda wako mwenyewe ni kwamba,unapaswa ukafanye maamuzi hayo wewe mwenyewe,yaani yawe yanatoka ndani yako kabisa.
Wazee wengi wamezoea kuishi peke yao licha ya kwamba jamii wanawaepuka kwa mfano; wazee hao wana uwezekano mkubwa wa kukaa peke yao kwa utulivu, bali sio rahisi wafaidike zaidi na hiyo hali yao ya upweke.
Lakini kwa watu ambao wako’bize’ ambao wanahusiana na wengine kila mara,kwao kuweka muda wa kuwa peke yao inakuwa ni fursa nzuri ya mapumziko na pia ya kujifanyia maboresho.
Ikiwa jambo la kuwa peke yako haikufuraishi, unapaswa uelewa kuwa ; kuwa peke yako ni ufunguo sahihi wa kutengeneza uzoefu chanya wa upweke huo. Kwa kutumia dakika chache ya ukimya unapaswa utumie vizuri muda huo kujichumbia mwenyewe hata kama ni mara moja kwa mwezi.
Kwa kujichumbia hivyo inakukumbusha ujifanyie kitu chenye tija kwako. Sio kwa sababu unakosa watu wa kujumiana nao ,bali ni kwa manufaa yako mwenyewe.
Kuna tafiti uliofanywa mwaka wa 2011,ulidokeza kwamba ‘ An exercise to teach the psychological benefits of solitude.’ Yaani watu wanaojichumbia wenyewe wanapata utulivu na ukimya na pia wanafurahia uhuru wa kufanya kile wanachotaka bila kuruhusu usumbufu wowote ule au kutarajia mambo fulani.
Wachache ambao hawakupata fursa ya kufurahia upweke huo wa kuwa peke yao,hawakuweza kufurahia uhuru huo wa utulivu. Lakini unapoongeza muda wa utulivu kwenye siku yako utafurahia na utapanga muda wa utulivu na ukimya kila mara.
Wakati wavuvi wanapovua samaki katikati mwa bahari ,huo ni muda mzuri sana kwao wa kupata amani na pia wa kufanya upya mawazo na fikra zako . Wengi wanakataa uzoefu huo na kuona kuwa ni wa kutosha sana .
Kwa kudharau kitu hutaweza kukaa nayo kwa muda mrefu. Ni muhimu kujishughulisha na mambo yanayoleta upweke kwenye maisha ambayo utafurahia kwenye kila siku ya maisha yako.
Kama unapenda asili, unapaswa uzingatie kutumia muda mwingi kwenye kufurahia mazingira na pia kutembea kwenye mapori. Kama unapenda chakula kizuri,unaweza ukapiga au uende kwenye mkahawa unaoupenda.
Hupaswi kukaa nyumbani tu ndio ufurahie upweke,badala yake chagua kufanya kitu ambacho huwezi ukafanya ukiwa na watu. Hakikisha haupo kwenye vitabu tu au unachati na mwenzako. Pointi nzuri hapa la kujichumbia mwenyewe ni kuhakikisha unakuwa peke yako na mawazo yako.
Mwandishi wako anayekujali sana.
Maureen Kemei.
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Jinsi ya kufanya uzoefu wa kuvumilia ukimya.
Wengi wetu tumezoea sana kusikia kelele nyingi kutoka pande zote. Hata inafika wakati mwingine watu wanatafuta njia mbalimbali za kuwafanya wasipaki peke yao wakiwa wametulia na mawazo yao.
Mtu yeyote anayelala wakati Tv ama redio inaongea , ukijaribu kuweka mawazo yako sawa , wakati unasikiliza kelele nyingi,hivyo sio afya nzuri kwako.
Kutengeneza dakika chache ya utulivu kwenye siku yako itakusaidia kwenye kuongeza nguvu zako . Chukua dakika kumi kila siku ukiwa umekaa chini huku umetulia na usijishughulishe na chochote bali unatulia huku ukifikiria.
Kama umezoea kelele na shughuli nyingi za kelele,kukaa kama umetulia kinaweza kusikuwe kuzuri sana kwako mwanzoni,lakini kwa kufanyia mazoezi kila siku kutakuwa sawa.
Unapaswa kuitumia wakati wa utulivu kufanya mambo yafuatayo:
Kwanza unapaswa upitie malengo yako. Unachukua dakika chache kila siku kufikiria kuhusu malengo yako. Fanya tathmini ya jinsi unavyoendelea na pia kutafakari namna unavyoweza kujifanyia maboresho au mabadiliko unayohitajika kufanya.
Pili zingatia hisia zako,fikiria kuhisi hisia zako na usongo wako wa mawazo. Chunguza kama ziko sawa ili uweze kutafakari njia za kuweza kujiboresha.
Tatu ni kuweka malengo yako wazi. Kamwe usiache kuota ndoto kubwa kuhusu kile unachohitaji, jinsi unavyotamani kesho yako kiwe. Njia rahisi ya kutengeneza kesho yako sasa ni kuamua aina gani ya maisha unahitaji.
Nne ni kwenye kuandika jarida lako. Uandishi wa journaling ni nzuri sana kwa sababu itakusaidia kuelewa zaidi na kujifunza kutoka kwenye hisia zako. Tafiti zinaonyesha kwamba kuandika kuhusu uzoefu wako wa kila siku na hisia zinazozunguka uzoefu wako zinakusaidia kwenye kuimarisha kinga za mwili na pia zinapungua msongo wa mawazo na pia kusaidia afya.
Tunaishi katika dunia ambayo kila siku tunaunganishwa na watu tofauti. Lakini kuunganishwa huku kitijidali inamaanisha kwamba tunapata fursa chache sana ya kukaa peke yetu na fikra zetu .
Kufikia simu yako ya mkononi na kuperuzi mtandaoni inachukua muda wako mwingi. Kuchukua muda wa mapumziko na kuacha kutumia teknolojia na kuweka muda mwingi kwenye kukaa kimya kwenye siku yako Kwa kujaribu kufanya yafuatayo;
- Kuzima Tv Yako kama unatumia
- Kuendesha gari yako bila kusikiliza redio.
- Kufanya matembezi bila simu yako ya mkononi.
- Kufunga eletroniki zote wakati mwingine na kupumzika.
Utulivu ni muhimu sana kwenye maisha yetu ya sasa ,kwa sababu utapata muda mzuri wa kutafakari maisha yako ,kuweka vizuri malengo yako na kuweza kujua dosari hivyo kujifanyia marekebisho mapema.
Mwandishi wako.
Maureen Kemei.
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Kwa nini tunadhani ulimwengu una deni letu.
Huwezi kushukuru kwa kitu ambacho unahisi una haki nacho Steven Furtick.
Kinachowatenganisha matajiri na masikini ni mtazamo wa haki. Mojawapo ya mtazamo ya watu masikini ni mtazamo wa haki. Mtu masikini ana hisia potofu na za uwongo za kustahiki. Wanaamini kuwa wana haki ya mambo mengi . Watu matajiri wana hisia kubwa ya shukrani,wakati masikini wana hisia kali ya haki na kwa hiyo , kuchukua mambo mengi kwa urahisi. Unapopoteza hisia zako za haki,unapata sababu zaidi ya kushukuru.
Inasemekana kuwa mawazo ya haki yamepunguza uwezo wa kiakili ya Kiafrika kufikiri kwa uwajibikaji na kimiliki maisha yao . Watu wenye mawazo ya haki daima wanaamini kwamba ulimwengu una deni kwao. Aina hii ya mawazo ina athari mbaya kwa maisha yao ya baadaye .
Yote unayoweza kupata kutoka kwa maisha ni vitu ambavyo unadai kutoka kwayo;hakuna mtu atakupa kile ambacho unastahili. Wewe Ndiye pekee unayeweza kuunda maisha unayotaka. Ni kupoteza udhibiti kamili kuwawajibisha wengine kwa hali hiyo katika maisha yako mwenyewe.
Kuna baadhi ya mabadiliko ya kitabia ambayo ni lazima tuyafanye Ili kupambana na athari inayodhoofisha ya mawazo ya haki katika maisha yetu. Nazo ni kama yafuatayo.
Kuwa na shukrani, Steven Furtick alisema kuwa “shukrani huanza pale ambapo hisia zangu za kustahiki huishia. “Mtu aliye na hisia za kustahiki huenda asiseme ‘asante’ au aonyeshe ishara nyingine za kuthamini kile alicho nacho. Hii ni kwa sababu wanaamini ni haki yao kuwa na kila kitu, hivyo hawathamini chochote. Shukrani hubadilisha mtazamo wako kutoka kwa kile ambacho unayakosa kwenye maisha yako kwenda kwenye utele ambao tayari upo.
Fanya kama ulimwengu hauwiwi chochote.:Elewa kwamba huna haki ya kupata chochote . Kwa bahati mbaya, ulimwengu hauna deni kwako . Maisha hayana haki na ni kazi yako kunufaika na kile unachopata maishani ,sio kulalamikia juu ya kile unachostahili lakini huna. Kadiri tunavyotambua mapema kwamba, hakuna mtu anayetudai chochote ndivyo bora kwetu na ndivyo tutakavyokuwa tayari kukabiliana na changamoto za maisha. Tunafanya kazi kwa kiwango cha juu cha uwajibikaji tunapojikumbusha kila mara kwamba hakuna mtu anayetudai chochote maishani.
Chukua wajibu kwa maisha yako :Jifunze kuwajibika na umiliki wa maisha yako ya baadaye . Albert Einstein alisema :”ikiwa unataka kuishi maisha yenye furaha ,fungamanisha na mradi,si watu wala vitu.” Watu wenye mawazo ya haki siku zote huamini kuwa matatizo yao si makosa yao na daima hujiona kama wahanga wa hali za maisha. Wanaamini sana kwamba mtu, kitu au serikali inawajibika kwa shida zao. Hawana uwezo wa kuwa waaminifu kwao wenyewe na kukubali kuwajibika kwa maisha yao. Hawawezi kuona jinsi hatua zao,vitendo ,kutotenda na uzembe wao vimewafikisha hapo ulipo. Ni makosa kuwajibishana wengine kwa hali hiyo katika maisha yako mwenyewe.
Amini kuwa wewe ni mwokozi wako mwenyewe. Sikia hii na ya wazi : Hakuna mtu anakuja kukuokoa . Wewe ni uokoaji wako mwenyewe ! Tishio kubwa kwa hatima yako ni Imani kuwa mtu mwingine atakuokoa .Barack Obama aliwahi kusema: ” Mabadiliko hayakuja ikiwa tutasubiri mtu mwingine au wakati mwingine . Sisi ndio tumekuwa tukingojea . Sisi ndio mabadiliko tunayotafuta . Lazima umiliki maisha yako ya baadaye. Chukua jukumu kamili la mahali ulipo sasa na unda mpango la mahali unapotaka kuwa . Kuwa na nia ya hatua ambazo utahitaji kuchukua hili kufikia pale unapotaka kuwa maishani. Badala ya kutafuta nanga ambazo ziko nje ya uwezo wako,anza kuchukua hatua.
Mtazamo wa haki ndio sababu kuu inayofanya watu wengi kuwa masikini, wasiofanikiwa ,wasiowajibika na wasio na shukrani. Watu matajiri wana hisia kali ya shukran, wakati masikini wana hisia kali za haki.
Ikiwa unataka kuunda matokeo tofauti na yale uliyopata hapo awali ,inabidi ujifunze kufikiri na kutenda tofauti . Ili kuishi maisha yenye mafanikio ,ni lazima tufute kabisa athari za mawazo ya kustahiki maishani mwetu.
Mwandishi wako.
Maureen Kemei
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Jinsi ya kujizoeza unyenyekevu kunavyokufanya uwe imara.
Mnamo mwaka wa 1940,Wilma Rudolph alizaliwa kabla hajamaliza miezi tisa ambayo mimba huwa inapaswa ikamilishe kabla ya mtoto kuzaliwa. Alikuwa na pounti nne tu,hivyo alikuwa mgonjwa tangu utotoni mwake.
Akiwa na miaka minne alipatwa na ugonjwa wa polio ambapo mguu wake wa kushoto ulikunjika kwa sababu alikuwa na shida ya leg bruce.
Kwa sababu hiyo alipaswa avae viatu vya orthopedic kwa miaka zingine miwili. Kwa usaidizi wa physical therapy , Rudolph aliweza kutembea vizuri akiwa na miaka 12 na kwa mara ya kwanza kwenye maisha yake ,akajiunga na timu ya wachezaji shuleni.
Aligundua kipaji chake cha kukimbia na upendo wake kwenye mchezo huo,alianza kufanya mazoezi. Akiwa na miaka 16,alipata nafasi kwenye uchezaji wa timu ya Olimpiki mwaka wa 1956. Akiwa mchanga kabisa kwenye timu hiyo alishinda medali kwa mbio iyo ya 4×100 relay. Baada ya hapo alirudi nyumbani na akazidi kufanya mazoezi zaidi kwa ajili ya Olimpiki ijayo.
Mwaka wa 1960 ,alijiunga na chuo kikuu cha Tennessee state ambapo aliweza kuendeleza mazoezi yake. Kwenye mwaka huo huo wakati wa mchezo wa Olimpiki, Rudolph akawa mwanamke wa kwanza nchini Marekani kushinda medali tatu ya gold kwenye Olimpiki moja. Alisifiwa sana na akawekwa kwenye historia, Rudolph alipumzika kutoka kwenye mchezo wa kukimbia akiwa na miaka 22.
Hata kama watu wengi wanalaumu shida na matatizo walizopitia wakiwa wadogo, Rudolph hakuwa hivyo. Hakupa nafasi chochote kimzuie hata ugonjwa ambao ulimsumbua tangu alipozaliwa. Hata hakulaumu uweusi wake kama mwanamke mweusi Marekani, au hakulaumu ufukara kwenye familia yake uliokuwa haujiwezi. Hata hivyo alijua kwamba dunia haiwezi ikamzuia yeye kufanya kile alichokipenda.
Rudolph alisema kuwa “haijalishi ni nini unataka kukamilisha,kikubwa ni nidhamu unayokuwa nayo. I was determined to discover what life held for me beyond the inner city-streets .” Hivyo ndivyo Rudolph alivyoenda tangu akitembea na mguu uliyowekwa pandeji hadi aliposhinda medali ya Olimpiki kwa muda wa miaka mitano tu.
Rudolph alipofariki mwaka wa 1994, legacy yake nzuri bado inaishi hadi sasa na bado inaendelea kuwapa wakimbiaji wengine tumaini waliopo na wajao.
Kuendelea kudhania kwamba umeumbwa Ili upate zaidi ya ulichonacho sasa haiwezi ikakusaidia chochote kwenye maisha yako. Unapoteza muda, uwezo wako inaweza kufanya ufe moyo mapema.
Unapochukua hatua ya kuacha kujionyesha ,na ukawa tayari kujifunza ,utakuwa tayari kujiboresha. Hivyo itakusaidia kwenye ufanisi wako kazini na kwenye maisha kwa ujumla.
Unapoacha hali ya kuona kwamba unataka zaidi na ukatosheka na kile ulichonacho, utapata mafanikio makubwa. Utaweza kusonga mbele kwa amani bila kuwa na msongo wowote. Kwa sababu utaona umetosheka lakini unatafuta mafanikio zaidi bila kuhisi uchungu wala kukata tamaa.
Mwandishi wako.
Maureen Kemei.
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin
-
Njia 3 ya kuwa Kocha wako mwenyewe.
Kama ilivyo kwa Kocha yeyote yule ambaye anakusanya mawaidha yaliyo bora na mazuri ,kwa ajili ya kukusaidia wewe ufikie kile ambacho unakitaka kwenye maisha yako.
Unapaswa pia uwe hivyo rafiki yangu kwenye safari hii ya kutafuta mafanikio. Unahitajika ujitoe vivyo hivyo kwako mwenyewe. Ona yale unayoweza ukafanya vizuri na uweke nguvu zako hapo ,chunguza eneo ambayo yanakuhitaji uboreshe na ujipe jaribio la kuwa bora zaidi.
Tafuta fursa za kujiboresha zaidi,lakini kwenye nyuma ya akili yako kaa ukijua na uelewe kwamba hutakuja kuwa bora zaidi. Unajaribu kuwa bora taratibu taratibu kwa kuzingatia njia tatu zifuatazo:
Njia ya kwanza ,chunguza tabia zako. Pata picha pale ambapo tabia zako zinashinda uwezo wako ,uwezo wa kujenga nguvu zako za akili. Kwa mfano ,kurudia kosa kisha tafuta mipango zitakazokusaidia ukae kwenye mchakato sahihi wa kujenga nguvu za akili .
Ya pili ni kuzawazisha hisia zako. Angalia wakati ambapo unajihurumia unapoogopa kufanya kitu ,unaogopa kuwa peke yako , hufurahii mafanikio ya wengine au hata unahofia kuwa hujaweza kufurahisha wengine.
Hupaswi kuruhusu hisia hizo zikurudishe nyuma,kumbuka ukitaka kubadilisha jinsi unavyohisi unatakiwa kubadilisha jinsi unavyofikiri na kubadilisha tabia zako zisizo nzuri.
Tatu ,fikiria kuhusu mawazo yako. Inakuchukua nguvu ya ziada na uwezo Ili kuelewa mawazo yako. Lakini kuwa chanya kupitiliza au hasi kupitiliza, huchangia jinsi unavyohisi na pia tabia zako na hata kuchangia kwenye nguvu zako za akili.
Chunguza kama mawazo yako ni ya kweli kabla ya kuamua ni nini unachotaka kufanya,hivyo hukusaidia kwenye kufanya maamuzi bora zaidi kwako.
Zingatia mawazo na Imani ambazo zinaweza kukurudisha nyuma,kama vile yale yanayochangia upeane nguvu zako,upoteze uwezo wako,kwenye mambo ambayo yaliyo nje ya uwezo wako,kukaa kwenye mambo yaliyopita,au kutarajia matokeo ya haraka. Badala yake badilisha hayo yote na mawazo yanayochangia kwenye kujenga mawazo chanya kwenye maisha yako.
Ni wazi kwamba hutaweza kubadilisha maisha ya kila mmoja. Ni uamuzi wa kila mmoja wetu, lakini badala ya kulalamikia watu hao ambao hawana nguvu za akili, jitahidi kuwa mfano bora kwao.
Unapaswa kufundisha watoto jinsi ya kuwa na nguvu za akili kwa sababu hawatafundishwa na dunia. Lakini jambo muhimu zaidi ni kujikaza kuwa bora zaidi kwako,na watu walio karibu na wewe wakiwamo watoto wako watagundua hilo.
Mwandishi wako.
Maureen Kemei.
http://www.uamshobinafsi.com/wp-admin