Mambo Ya Kujifunza Kutoka Kitabu Excellence Advice For Living.

  1. Kuwa na shauku ni sawasawa na kuongeza 25% kwenye akili.
  2. Mara zote taka jambo la mwisho, kuwa na dead line kwa kila jambo.
  3. Samehee hii ni kwa ajili yako mwenyewe.
  4. Usipime maisha yako kwa kutumia rula ya mwingine.
  5. Sehemu kubwa ya kusafiri ni kuacha mambo mengi nyuma.
  6. Lengo bora unaloweka kwenye mwaka ni kujifunza kitu kimoja kwa kina zaidi.
  7. Maumivu hayakwepeki kuteseka ni kuchagua.
  8. Kama unatafuta kitu ndani alafu hukioni ukikipata usikirudishe hapo kirudishe ulipoanza kukitafuta.
  9. Unapaswa kuchagua kitu kimoja ambacho unachokitak zaidi ya vyote kukifanya.
  10. Njia bora ya kujifunza kitu ni kuwafundisha wengine.
  11. Kanuni ya ukuu ni kuwa bora zaidi kila siku alafu rudia kila siku.
  12. Unapokuwa njia panda chagua njia inayoleta mabadiliko.
  13. Unaweza kutegemea tabia zaidi kuliko hamasa.
  14. Unapaswa kutaka ushahidi usio wa kawaida ili upate matokeo yasiyo ya kawaida.
  15. Usiwe bora kuwa wa kipekee .
  16. Usichukulie binafsi, wachukulie kama wewe.
  17. Fanya kitu kizuri , na ufanye tena na tena na tena.
  18. Boresha akili yako, fikiria kwa miguu,fikiria kwa mikono, tembea, andika.
  19. Punguza orodha yako ya vitu unavyofanya.
  20. Wajibika kwa makosa yako.
  21. Weka nguvu zako kuwahudhumia wateja wako kuliko kushindana na washindani.
  22. Hapana ni jibu tosha.
  23. Kama huanguki mara kwa mara hutembei unazurura, au hujionei aibu kwa mambo ya zamani basi hukui.
  24. Asilimia 99 ya mafanikio ni kuongea na mteja, kumpigia simu, onekana mara zote.
  25. Usiwe na haraka, ukiwa na haraka ndio utaibiwa, utatapeliwa.
  26. Hakuna ukomo wa kuwa bora, kuna kitu cha kuboresha kila siku.
  27. Usipoteze changamoto , penye changamoto ni sehemu ya kukua na kupiga hatua.
  28. Wewe ni kile unachofanya.
  29. Angalia maslahi unapoomba ushauri.
  30. Jambo unaloliona ni la kitoto ndilo linaweza kukufanikisha, bobea kwenye kile unachokifanya.
  31. Ukikopesha kitu, chukulia unampa zawadi, kama hatarudisha hutaumia.
  32. Kuwekeza hela kidogo kunaleta miujiza.
  33. Usikubali haraka ya mtu iwe dharura. Fanya kulingana na umuhimu sio dharura.
  34. Ukiona mtu analazimisha kitu, jua Kuna uongo nyumba yake.
  35. Kama hujishangai yale uliyokuwa ukitenda uko nyuma, basi usishangae ya mwenzio.

Rafiki tuifanyie kazi mambo haya na tutazidi kuwa bora kila siku kwenye maisha yetu.

Rafiki yako,

Maureen Kemei.

kemeimaureen7@gmail.com

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment