Home

  • Jinsi ya kushughulikia kinyongo dhidi ya mtu.

    Unaweza achia.

    Kuna sababu nyingi ambazo unaweza kumchukia mtu,huenda alikuumiza zamani,unaweza kuhisi kana kwamba anakunyang’anya,au unaweza kuhisi wivu kwamba ana baadhi ya Mambo unayotaka maishani.

    Walakini ,kushikilia hasira na chuki Kwa mtu mwingine kunaweza kuanza kukumaliza. Kwa bahati nzuri,ikiwa uko tayari kufanya kazi, unaweza kuanza kushughulikia hisia hizo kwa njia ambayo ni ya afya kwako,na unaweza hata kupata kwamba unaweza kukubali yaliyopita na kumsamehe mtu mwingine.

    Kukubali na kuhisi hisia zako. Ruhusu kuhisi hisia zako badala ya kuzipuuza. Unaposhughulikia hisia hasi kama vile kukataliwa,hasira,kukatishwa tamaa,wivu au kuumizwa, unapaswa ujipe ruhusu ya kuzihisi kweli.Kujaribu kusukuma hisia hizo chini kutazifanya zijengeke ndani yako. Na hatimaye,hiyo ndiyo husababisha hisia za chuki.Unapojiruhusu kupata hisia hizo,kwa upande mwingine, ni rahisi kuziachilia baadaye.

    Jiulize ni nini kinasababisha chuki yako. Ni nini hasa kilikufanya uhisi hivi? Wakati mwingine sabuni ya chuki yako inaweza kuwa wazi,kama mtu mwingine alikuumiza wazi wazi katika siku za nyuma.Nyakati nyingine ni vigumu zaidi kujua ni nini hasa kinakusumbua. Chuki yako inaweza kuwa imeongezeka kwa muda mrefu,au unaweza kumchukia mtu kwa sababu ana kitu unachotaka.

    Fanya mpango wa utekelezaji kwa siku zijazo. Wakati fulani, jinsi unavyoshughulikia hali fulani kunaweza kuongezea kinyongo chako. Kwa mfano,unaweza kuhisi kama ulipaswa kujitetea ikiwa mtu fulani alikudharau au hakukuunga mkono. Badala ya kujipiga teke Kwa kile ambacho hukufanya,panga jinsi unavyoweza kukabiliana na hali kama hizo katika siku zijazo.Si tu kwamba hili itakusaidia kuepuka chuki zaidi baadaye,lakini kuchukua mbinu makini kunaweza kukusaidia kuacha baadhi ya hisia unazozishikilia sasa.

    Acha mawazo yako hasi katika nyimbo zao. Ukiona unarudia tena tena kuhusu maumivu ya zamani,jikumbushe kuangazia jambo lingine ,kama vile chochote kinachotokea sasa au kitu ambacho unaweza kufanyia ili kuepuka hali hiyo katika siku zijazo .Inaweza kuwa ngumu sana kubadilisha mifumo yako ya kufikiri ,hasa kwa sasa ,lakini endelea kijaribu,inakuwa rahisi Kwa mazoezi.

    Andika hisia zako. Kuandika ni njia nzuri ya kupanga mawazo yako,na inaweza kukusaidia kupata mizizi wa chuki yako. Usijali kuhusu kuweka mambo chini kwa mpangilio wowote kamili,andika tu mawazo yako yanapokujia. Andika kuhusu Kwa nini umemkasirikia mtu fulani, jinsi inavyokuathiri Leo,na matukio yoyote ya zamani ambayo yanafanya hili kuumiza zaidi.

    Zungumza na mtu kuhusu jinsi unvyohisi. Wasiliana na rafiki au mwanafamilia unayemwamini. Fungua kinyongo chako ongea kuhusu jinsi kilikufanya uhisi na kwa nini bado kinasumbua. Sio tu kwamba utajiskia vizuri mara tu unapoondoa hisia zako kwenye kifua chako, lakini kuzungumza kunaweza kukusaidia kuona hali kwa mtazamo tofauti. Mtu unayezungumza naye anaweza pia kukupa maarifa muhimu.

    Hatua ya kuchukua;kuweka kinyongo ni sawa na kunywa sumu na kungoja mtu mwingine afe. Kwa hivyo ni vizuri kuzingatia njia za kupunguza msongo na hatimaye utaishi maisha ya furaha na ya kuelewana na watu, asante.

    Mimi mwandishi na mshauri wako.

    Maureeen Kemei.

    Mawasiliano:

    www.uamshobinafsi.com.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Umuhimu wa kujijua mwenyewe.

    Nini maana ya kujijua.

    kujijua ni juu ya kugungua ni nini kinachokufanya uwe salama.

    Miongoni mwa mambo mengine,inamaanisha:

    kujifunza mambo unayopenda na usiyopenda.

    Kufunua imani na maadili yako.

    Kujua mipaka yako ya kibinafsi.

    Kukubali sifa zako za kibinafsi.

    Kuwa mchezaji bora wa timu.

    Kuwa na njia iliyo wazi zaidi katika maisha yako ya kitaalamu.

    Kuelewa jinsi unavyowasiliana na wengine.

    Kutambua maadili yako ya msingi ya kibinafsi.

    Kuongeza uwezo wako wa kujihurumia.

    Kuwa na wazo wazi la kusudi la maisha.

    Kujua nini kinahitajika ili kuwa na motisha binafsi.

    kubadilika zaidi.

    Kujitambua zaidi kunasaidia kujiendeleza ,kukubalika,na kuwa makini huku tukinufaisha afya yetu ya akili kwa ujimla.

    Hatua ya kuchukua,kwa kujijua sisi wenyewe tutakuwa na ujasiri zaidi,tutafanya maamuzi bora zaidi, tutakuwa na uhusiano thabiti na kuwa waaminifu zaidi.

    Akujaliaye sana.

    Mwandishi Maureen Kemei.

    mawasiliano:

    kemeimaureen7@gmail.com.

    www.uamshobinafsi.com.

  • Maana ya uamsho binafsi.

    Unawezaje fanya uamsho?

    Rafiki mpendwa , karibu kwenye mada wetu leo ambapo tunazungumzia kuhusu uamsho wa mtu binafsi.

    Kwanza kabisa tunaangalia maana ya uamsho binafsi ,uamsho binafsi ni hali ya kuweka mkazo kwenye mambo ya ndani zaidi kuliko mambo ya nje,hali ya kuuuliza,kudadisi mambo na kujipa changamoto fulani.

    Watu wanaofanya uamsho hawategemei mazingira ya nje kuwa wanachangia nini kwenye furaha yao ya ndani. Yaani watu hao wanaamini uwezo wao wa ndani na wanatumia uwezo huo katika maisha yao ya kila siku.

    Wakati wa kusuluhisha changamoto fulani au hata wanahisi kuwa na nguvu wakati wa magumu.Wanaojiamsha wanaelewa kabisa namna ya kujiponya kutokana na magumu au changamoto yoyote yale wanayopitia.

    Wanatafuta njia mbali mbali ambao wanaona wanaweza ikawanufaisha katika maisha yao ya kila siku.Kama kuamka kifedha,kiroho,kimwili,kikazi nk.

    Wanaendeshwa na kusudi lao kuu la maisha na hawakatishwi tamaa hovyo na wengine au hali fulani maana wameshajua kusudi lao la maisha.

    Wanapenda kuwa huru na kujitegemea,badala ya kukubali kushindwa na majaribu au magumu wowote ule unaowakabili.Wanatafuta njia ya kusuluhisha changamoto hizo au wanatumia changamoto hizo Kama fursa ya wao kupiga hatua zaidi.

    Wanaamini uwezo ulio ndani yao na kwamba wanaweza wakatumia uwezo huo kufanya makubwa katika maisha yao.

    Hatua ya kuchukua; katika kujifanyia uamsho ni wewe mwenyewe unayechukua hatua huo. Hakuna atayekulazimisha lakini unapoamua kujiamsha unapaswa kufahamu kwamba utakataliwa na watu wengi hata jamaa wako wa karibu.

    Unapaswa kuelewa hayo kabla ya kuamua kujifanyia uamsho.Asante rafiki wangu karibu tuendelee pamoja kwenye kujifunza swala hili.

    Akujaliaye sana.

    Mwandishi Maureen Kemei.

    mawasiliano:

    kemeimaureen7@gmail.com

    www.uamshobinafsi.com

  • Matatizo 7 yanayotokana na kufikiria yaliyopita.

    We do not heal the past by dwelling there ;we heal the past by living fully in the present. Marianne Williamson.

    Kwanza ni kwamba huwezi ukaishi kwenye wakati uliopo. Huwezi furahia wakati uliopo kama bado akili na hisia zako zinafikiria yaliyopita. Kwani hutaweza kuchangamkia fursa mpya na pia kufurahia wakati uliopo.

    Kukaa kwenye mambo yaliyopita yanakufanya uone kujitayarisha kwa yajayo kama ni ngumu. Unaona kabisa ni ngumu kwako kuweka malengo yako vizuri au kukubali mabadiliko kama bado kiasi kikubwa ya fikra yako, yako kwenye yaliyopita.

    Yanakuzuia kufanya maamuzi sahihi. Ukiwa na mambo ambayo hujasuluhisha yatakuzuia usifikirie kwenye kufanya maamuzi au hutaweza kufahamu kilicho kizuri kwako.

    Kukaa kwenye yaliyopita hakiwezi kukusaidia chochote. Utaendelea kufikiri vilevile katika akili yako na utafokasi kwenye mambo ambayo hayawezi badili chochote.

    Kudhani yaliyopita yalikuwa mazuri kuliko ya sasa. Ni rahisi kujirai kwamba yaliyopita yalikuwa nafuu kuliko ya sasa. Unaweza dai kwamba ulikuwa unajiamini zaidi kuliko sasa, haukuwa unaumizwa sana kama sasa. Yanakufanya uone jinsi mambo yalivyokuwa mazuri na yalivyo mabaya sasa.

    Kufikiria zaidi mambo yaliyopita sio nzuri kwa afya yako. Kuwa hasi wakati wote inachangia kuungua kwa mwili wako, huu ni kulingana na uchunguzi uliofanywa na wataalamu mnamo mwaka wa 2013. Ulifanywa katika chuo cha Ohio, ilijulikana kwamba kufikiria yaliyopita yanakuweka kwenye hatari ya kupata magonjwa kama ya moyo, saratani na dimensia.

    Hatua ya kuchukua, rafiki yangu kama ambavyo tumejifunza shida yanayotokana na kusumbuliwa na mambo yaliyopita, ni muhimu kwetu kukataa mambo hasi na yasiyofaa maana tusipofanya hivyo yataendelea kupoteza nguvu na muda wetu bila kufanya chochote chenye tija kwenye maisha yetu.

    Kutoka kwako akujaliaye sana.

    Mwandishi, Maureen Kemei.

    Mawasiliano

    Kemeimaureen7@gmail.com

  • Njia unazoweza kutumia kujifunza kuwa na fikra wazi.

    Tumia maumivu kama mwongozo wa kukusaidia kufanya tafakari na tathmini ya usahihi wa kile unachoamini au kusimamia. Pale makosa au udhaifu wako vinapoguswa, unapata maumivu, yatumie maumivu hayo kuchukua hatua sahihi.

    Jijengee tabia ya kuwa na fikra wazi. Maisha unayoishi, yanayokana na tabia ambazo umejijengea. Ukijijengea tabia ya kuwa na fikra wazi, kuwa tayari kujifunza na kubadilika, hayo ndiyo aina ya maisha utakapokuwa nayo.

    Jua upofu wako ulipo. Angalia makosa ambayo umekuwa unafanya kwa kujirudia, pia waulize wengine wakuoneshe madhaifu uliyonayo ili uweze kuyaona na kuchukua hatua sahihi.

    Kama watu wengi wanaoaminika wanasema unakosea, halafu wewe pekee ndiye unayeamini unafanya kwa usahihi, ni wakati wa kujifikiria, kuna uwekezekano mkubwa kwamba unakosea. Chukua wao na jiulize ni wapi unaweza kuwa unakosea ili uweze kuuona ukweli.

    Fanya tahajudi meditate. Tahajudi inakusaidia kutuliza fikra zao, hasa kwenye nafsi yako ya chini na kukuwezesha kuwa tulivu na kuona vitu jinsi vilivyo na siyo unavyotaka wewe viwe. Tahajudi imakuwezesha kukabiliana kwa tulivu na hali yoyote, hata kama ni ngumu na kubwa kiasi gani.

    Ongozwa na u|shahidi evidence – based na wawezeshe wengine kuwa hivyo. Chochote unachoamini au kukubaliana nacho kwamba ni kweli, unapaswa kuwa na ushahidi unaopaswa kuuonesha kwamba ni kweli.

    Jua ni wakati gani wa kuacha kupingana na kukubaliana kulingana na mchakato uliowekwa. Kuna wakati mabishano baina yako na mwingine hayatafikia tamati, kila mtu ataendelea kuamini kwenye upande wake. Katika hali kama hii, kuendelea ni Kupoteza muda. Badala yake unapaswa kufuata mchakato sahihi, labda ya kwenda Ngazi ya juu kwa kumhusisha mtu ambaye ni mtaalamu au mwenye uzoefu zaidi.

    Hatua ya kuchukua kupitia msingi huu unapaswa kuwa tayari kukabiliana na changamoto mbalimbali ili kuweza kuujua ukweli, iwe unatoka kwako au kwa wengine.

    Lakini hii haimaanishi kwamba unakubaliana na wengine kirahisi, bali unakubaliana nao wanapokuwa na ushahidi wa ukweli kuliko wewe.

    Akujaliaye sana.

    Mwandishi, Maureen Kemei.

  • Chanzo cha matatizo.

    Kosa kubwa ambalo watu wengi wanalifanya kwenye siku zao ni kupoteza muda na nguvu kwenye mambo yasiyo na tija.

    Wengi wanafanya kazi au biashara ambazo hawazipendi. Hivyo wanachelewa kuanza kazi na kuwahi kumaliza.

    Lakini pia wakati wa kufanya, wanaingiliwa na usumbufu mwingi kitu ambacho kitu kinachofanya ufanisi wao kuwa mdogo. Kwa kifupi japo mtu huyu anakuwa kwenye kazi, hatumii nguvu zake zote kwenye kile anachofanya.

    Lakini sasa, siku ya kazi inapoisha anajiambia amechoka na hawezi kufanya kitu kingine. Haangalii masaa mengine nje ya hiyo ya kazi, ambayo ni mengi kuliko yale ya kazi.

    Ufanyaji kazi wa wengi siyo wenye tija kwamba kuna matokeo anataka kuzalisha. Mtu anafanya tu ili amalize au muda uende. Pamoja na kufanya kazi mbovu kwenye theluthi moja ya muda wake, bado anapoteza theluthi nyingine mbili.

    Kama mtu anataka kweli kuishi kwa ukamilifu na kufanya makubwa, ni lazima atengenese siku ndani ya siku, yaani awe na siku mbili ndani ya siku moja.

    Siku ya kwanza ni ile ya kazi inayoanza saa mbili asubuhi mpaka saa kumi jioni. Na siku ya pili ni ile binafsi nje ya kazi inayoanza saa kumi jioni mpaka saa mbili asubuhi.

    Siku ya kwanza ambayo ni ya kazi ina masaa 8,siku ya pili ambayo ni binafsi ina masaa 16. Unaweza kujionea hapo kwamba kila mtu ana muda mwingi nje ya muda wa kawaida wa kazi au biashara.

    Wengi hupoteza hayo masaa ya nje ya kazi wakijiambia wanapumzika. Lakini ukweli ni kwamba kazi za wengi ni za kutumia akili kuliko nguvu na akili huwa haipumziki, bali inabadili vitu vya kufanya hili kuondoa hali ya uchoshi.

    Hatua ya kuchukua akili haichoki kama misuli, hivyo tofauti na kulala haihitaji mapumziko, bali inahitaji mabadiliko. Ukifanya kitu kimoja kwa muda mrefu akili inakichoka.

    Ukikiacha hicho na kufanya kitu kingine akili inakuwa na nguvu za kutosha, hata kama ni kitu kigumu.

    Akujaliaye sana.

    Mwandishi, Maureen Kemei.

    Fikrachanya.wordpress.com

  • Njia ya kuelekea kwenye uhuru.

    Njia ya kuvuka utumwa ni kwenye kupata uhuru wa muda. Hii ni njia ya Ustoa ambao wanafalsafa kama Seneca aliamini kuwa uhuru kamili kwenye maisha ni uhuru wa muda.

    Pale mtu anapoweza kudhibiti na kupangilia muda wake ndiyo anaweza kuwa na uhuru wa maisha. Kwenye kila mwanzo wa barua yake kwa Lucillus, Seneca alimsisitiza aendelee kujiweka huru kwa kuchukua udhibiti wa muda wake ambao alikuwa ameupoteza kwa muda mrefu.

    Kama unapoteza muda au kama muda wako unadhibitiwa na watu wengine basi jua haupo huru. Wale wanaodhibiti muda wako ndiyo wamekufanya kuwa mtumwa wao.

    Wastoa pia waliamini ni wenye hekima pekee ndiyo wanaoweza kuwa huru. Wakiamini mtu asiye na hekima huishia kusumbuliwa na hisia mbalimbali zinazomfanya asiwe huru.

    Na pia Seneca anasisitiza watu wengi hawapo huru siyo wa sababu wameshikiliwa kwa lazima kwenye utumwa, bali kwa sababu wao wenyewe wameushikilia utumwa kwa lazima. Yaani hawataki kuachilia vitu ambavyo vinawanyima uhuru.

    Hii ndiyo hali iliyopo sasa, ambapo japokuwa kila mtu yupo huru kimwili, kisaikolojia wengi wawejishikilia kwenye utumwa wa aina mbalimbali.

    Hatua ya kuchukua ni wakati sasa wa kuondokana na kila aina ya utumwa tuliopo na kuwa huru. Kwa kuanza na kudhibiti muda wetu na kujijengea hekima ya kuweza kukabiliana na kila jambo kwenye maisha.

    Akujaliaye sana.

    Mwandishi wako.

    Maureen Kemei.

  • Jinsi ya kuua sauti ya ndani inayokukatisha tamaa.

    Kila mmoja wetu huwa ana sauti ya kukatisha tamaa ambayo ipo ndani yake. Ni sauti hiyo ndiyo huwa kikwazo kwa wengi kufanya makubwa.

    Hakuna asiyeweza kuijua ni nini anapaswa kufanya ili apate anachotaka. Ila wakati wa kufanya kitu hicho unapofika, sauti ya ndani inawashawishi na wanaishia kutokufanya.

    Kwa mfano unaweza kuipanga vizuri kabisa kwamba kesho utaamka asubuhi na mapema. Unaweka kabisa alamu kwenye simu yako kwamba muda ukifika ikuamshe.

    Muda unafika, alamu unaita, unaisikia kabisa, lakini sauti ya ndani inaanza hadaa yake. Sauti hiyo inakuambia ulale kidogo ndiyo uamke, inakushawishi kwamba jana ulichoka sana. Inakuhadaa kwamba unahitaji dakika tano tu za ziada za kulala halafu utaamka.

    Unajua unapoisikiliza sauti hiyo, unakuja kuamka saa moja au mawili baadaye, umeshachelewa na mipango uliyokuwa umeweka uikamilishe mapema inakuwa haiwezekani tena.

    Bila kuiua sauti hiyo ya ndani utapanga, mambo mengi sana, lakini hakuna lolote utakalokamilisha. Maana sauti hiyo haitaki kukuona ukiteseka, itatumia kila ushawishi kuhakikisha husumbuki na mambo makubwa.

    Sauti hiyo ya ndani ipo ndani ya kila mtu, tumekuwa nayo kwa miaka yetu yote. Ni sauti yenye nguvu kubwa ya ushawishi kwetu, kwa sababu inajua sana udhaifu wetu.

    Inabidi ujue sauti hiyo kwa sababu ukiiacha hai, huwa haichoki, Itaendelea kukushawishi na hasa kukukamata kwenye udhaifu wako na hapo utajikuta umehadaika na sauti hiyo ya ndani na kutokufanya kile unachojua ni muhimu kufanya.

    Kuijua sauti hiyo unapaswa kutaka sana kile unachotaka kiasi kwamba hakuna namna utakwamishwa na chochote. Macho yako na umakini wako wote unakuwa kwenye kile unachotaka kiasi kwamba mengine yote yanakosa maana kwako.

    Hatua ya kuchukua, unapaswa kuwa bize sana na kile unachotaka kiasi kwamba sauti hiyo ya ndani inakosa kabisa nafasi. Kila inapotaka kuja kwako hakuna mahali inapata nafasi.

    Msukumo wako kwenye kile unachotaka unakuwa mkubwa mno kiasi kwamba hakuna chochote kinachokuyumbisha. Unachokuwa unataka ni kile unachotaka na hakuna kingine chenye nafasi.

    Akujaliaye sana.

    Mwandishi wako.

    Maureen Kemei.

  • Kinachokupa hofu ndiyo unapaswa kukifanya zaidi.

    Chochote kinachokutisha unapaswa ufanye zaidi, Derek kwenye kitabu chake cha” Hell yeah or No. “anatuambia kuwa ana kauli mbiu mpya anayoiishi kwenye maisha yake, ambayo ni hii :chochote kinachokutisha ndiyo unapaswa kukifanya zaidi.

    Anatuambia kwa miaka 30 amekuwa akiifuata kauli mbiu hiyo na imemwezesha kufanya makubwa sana.

    Chochote unachotaka, ila inakutisha au kukupa hofu, ni kiashiria kwamba hicho ni kitu sahihi kwako. Hivyo usiogope na kuacha, badala yake kikabili. Hapo ndipo kwenye ukuaji na mafanikio.

    Ukweli ni kwamba, unapokikabili kile kinachokutisha, hukiogopi tena. Unapata ujasiri mkubwa wa kuendelea kukifanya kwa viwango vya juu zaidi.

    Mwanasaikolojoa Abraham Mascow amewahi kunukuliwa akisema :”Maisha ni mchakato endelevu wa kuchagua kati ya usalama (kwa kuhofia na kujilinda) na hatari (kwa kupiga hatua na kukua).” Chagua zaidi ukuaji kuliko hofu.

    Hatua ya kuchukua ;kwa kuchagua zaidi ukuaji kuliko hofu, ndivyo unavyopaswa kuyaishi maisha yako, chochote kinachokutisha au kukupa hofu, ndiyo unapaswa kukifanya zaidi.

    Akujaliaye sana.

    Maureen Kemei.

  • Kujitambua.

    Kikwazo kikubwa kinachofanya watu kushindwa kuishi maisha halisi kwao ni kutojitambua na hivyo kujikuta wakiiga watu wengine.

    Na hilo limekuwa hatari sana kwenye zama hizi ambapo ushauri wa maisha umekuwa mwingi. Wengi wanajikuta wakiiga wengine kwa namna mbalimbali hivyo licha ya kuweka juhudi na muda, bado hawafanikiwi.

    Ni muhimu kujitambua sana wewe mwenyewe ili uweze kuishi maisha halisi kwako. Ustoa unasisitiza sana tujitambue sisi wenyewe ili tusisumbuke na mambo yasiyo sahihi kwetu. Maana Kuna mambo wengine wanaweza kufanya na wakafanikiwa vizuri, ila sisi tukafanya tusifanikiwe.

    Hatua ya kuchukua, hili kuepuka kupoteza muda na nguvu, tujitambue na kuishi kulingana na upekee na utofauti wetu.

    Kuiga maisha ya wengine ndiyo chanzo cha wengi kuwa na maisha magumu.

    Akujaliaye sana.

    Maureen Kemei.