Home

  • Jinsi hofu ya kupitwa inavyokutesa.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini katika ulimwengu wa sasa ambao zaidi ya asilimia 99, ya watu hulala na simu zao kitandani.

    Lakini pia takwimu zinaonesha kuwa asilimia 80 ya watu hushika kwanza simu zao na kuangalia habari, na taarifa mbali mbali kabla ya kuamka na kutoka kitandani.

    Simu ndiyo inakuwa kitu cha mwisho kushika wakati analala na cha kwanza kushika pale anapoamka . Imekuwa ni kama sehemu ya kiungo cha mwili wa mwanadamu.

    Si hivyo tu, mtu yuko tayari kushika simu na kujua yanayoendelea mtandaoni na ulimwenguni, lakini hajui hata kama mguu wake ni mzima.

    Achilia mbali kama amelala na mwenza wake ndio kabisa, ataanza kujua yanayoendelea huko kitandani kabla ya kujua hali ya mwenza wake huyo aliyenaye karibu.

    Hali hii inatokana na hofu ya kupitwa na yale yanayoendelea mtandaoni. Hutaki kupitwa unataka uwe wa kwanza kujua kila kitu kinachoendelea ulimwenguni.

    Mitandao ya kijamii na hata vyombo vya habari wanajua siri hii. Unahofu ya kupitwa na habari, na matukio mbali mbali yanayokuwa yakiendelea mtandaoni . Ukipitwa unajiskia vibaya. Na hivyo wanatumia mtego huo kukunasa.

    Ili uweze kujinasua katika mtego huu unapaswa, kuitawala hofu yako ya kupitwa na yale yanayoendelea mtandaoni. Uitawale hofu yako kwa sababu, usipofanya hivyo wenyewe mtandao na vyombo vya habari wanaitumia hofu yako hiyo kwa faida yao wenyewe.

    Siyo kila taarifa au habari zinakufaa wewe kuzijua. Kama habari au taarifa haikuongezei maarifa au fundisho, jua kuwa haikufai.

    Mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kama vile runinga, redio na magazeti, vinawinda umakini wako. Umakini wako ilipotea, muda na nguvu zako pia zinapotea, hivyo hutaweza kutimiza malengo na maono uliyonayo.

    Kuchukua hatua rafiki yangu, tunapaswa kuitawala hofu ya kupitwa ili tusipoteze nguvu na muda wetu kwenye mtandao na habari mpasuko, kwani hatutaweza kutimiza malengo yetu.

    Akupendaye sana,

    Maureen Kemei .

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Jinsi ya kuitawala hofu yako.

    Rafiki yangu mpendwa, hofu imekuwa kikwazo cha watu wengi kufikia mafanikio yao. Hofu imewazuia watu wengi kufanya maamuzi kama, kuanzisha biashara, kupata kazi, kuzikimbiza ndoto zao na hata kutimiza malengo. Hofu ni kama kansa, ikiwa eneo moja husambaa na kuenea kwenye maeneo yote ya maisha ya mtu.

    Ukiwa na hofu ya kuongea mbele za watu leo, baada ya muda hofu hiyo itaenea kwenye maeneo yote ya maisha, mahusiano, kazi na hata eneo la mafanikio.

    Kuna namna bora ya kuitawala hofu yako.

    Hatua ya kwanza katika kuitawala hofu yako ni wewe kujua kwamba unahofu ya kitu, jambo au mambo fulani. Kutambua kuwa kuna kitu huwa unahofia. Mara nyingi badala ya faida, manufaa au maumivu wa kitu au jambo unalolihofia.

    Hatua ya pili ni wewe kujua chanzo kikuu cha hofu yako hiyo. Kama unahofu ya kusimama mbele ya watu kuongea, unapaswa kujua chanzo cha hofu hiyo.

    Hatua ya tatu ni kufanya kile unachokihofia na kukiogopa. Ukishajua hofu yako, chanzo kikuu na vichocheo vya hofu yako ni jukumu lako kufanya kile unachokihofia na kukiogopa.

    Kwanza unatakiwa kuondoa kumbukumbu mbaya na hatarishi za kitu au jambo unalolihofia na kuliogopa.

    Kuchukua hatua rafiki yangu ili kuweza kushinda hofu acha kutanguliza madhara badala yake tanguliza faida, manufaa na umuhimu wa kitu au jambo unalopaswa kulifanya.

    Akupendaye sana,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Mambo 3 ya kujenga kumbukumbu.

    Rafiki yangu mpendwa kumbukumbu ni hitaji muhimu kwenye kuendesha maisha yetu ya kila siku.

    Hebu fikiria kama kila siku ungekuwa unaamka ukiwa mpya bila kumbukumbu yoyote na inakubidi ujifunze kila siku, maisha yangekuwa magumu sana.

    Lakini kwa kuwa una kumbukumbu ya mambo mengi, maisha yanakuwa rahisi. Ili kuondoa ukomo kwenye maisha yako, lazima uondoe ukomo kwenye kumbukumbu zako.

    Ili uweze kukumbuka kitu chochote kwa urahisi, unahitaji mambo hata matatu muhimu.

    Moja motisha. Unakumbuka zaidi kitu ambacho kina motisha kuliko ambacho hakina. Mfano mtu akikuambia nitafute kesho saa tano unaweza ukasahau . Lakini akikuambia nitafute saa tano nikupe millioni moja huwezi kusahau. Hapo kuna motisha unaokufanya ukumbuke. Kwa kila unachotaka kukumbuka, kiwekee motisha utakaokusukuma ukumbuke.

    Mbili ni umakini. Unaweza kukumbuka kile ambacho umekipa umakini wako. Kama hujaweka umakini kwenye kitu, inakuwa vigumu kukukumbuka. Kwa kila unachotaka kukumbuka, kiwekee umakini mkubwa.

    Tatu ni njia unazotumia kujifunza kitu na hata kukikumbuka. Kwa wengi hutumia njia ya kukariri, ambayo inachosha na kusahau haraka.

    Kuchukua hatua, sina uhakika kama itakufaa, lakini wale wanaokumbuka mengi ni kwa sababu wanatumia ubongo wao. Na wanaosahau hawatumii ubongo wao. Leo chagua kutumia ubongo wako rafiki yangu.

    Akupendaye sana.

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

    Uamshibinafsi.com.

  • Manufaa 6 yanayotokana na usomaji wa vitabu.

    Rafiki yangu mpendwa zipo njia nyingi sana ya kujifunza,lakini njia bora kabisa ni ya kusoma. Sina uhakika kama itakufaa, lakini watu wote waliofanya makubwa kwenye maisha yao, ni wasomaji wakubwa.

    Ipo kauli inavyosema viongozi ni wasomaji. Hakuna kiongozi bora ambaye siyo msomaji wa vitabu. Changamoto kubwa kwenye usomaji ni kwamba bado watu wanasoma kizamani.

    Kipindi cha nyuma maarifa hayakuwa mengi kama sasa, hivyo watu walijifunza taratibu. Lakini kwa zama tunazoishi sasa, maarifa ni mengi mno na mengi ni muhimu. Kuendelea kusoma kwa mazoea ni kujiwekea ukomo kwenye kupata maarifa hayo mazuri.

    Usiwe na wasiwasi rafiki yangu hapa tunakwenda kujifunza jinsi ya kuondoa ukomo kwenye usomaji kwa kujifunza jinsi ya kusoma haraka na kuelewa pia.

    1. Usomaji unakuza na kukomaza ubongo wako. Unapojifunza kitu kipya ubongo wetu unatengeneza muunganiko mpya wa mishipa ya fahamu. Kwa kusoma na kuandika ubongo wako unakua zaidi.
    2. Usomaji unaboresha kumbukumbu zako. Wasomaji huwa wanakuwa na kumbukumbu nzuri kuliko wasio wasomaji.
    3. Usomaji unaboresha umakini wako. Unaposoma, fikra zako zote zinakuwa kwenye kile unachosoma na hilo linakufanya uwe makini zaidi.
    4. Usomaji unamwongezea mtu misamiati mipya ambayo inamfanya aweze kuelewa vizuri na hata kuwasiliana na watu vizuri. Tafiti zinaonesha kipato cha mtu kinaendana na kiwango cha msamiati anayojua.
    5. Usomaji unaboresha uwezo wako wa kujenga taswira. Unaposoma unajijengea picha kwenye akili yako ya kile unachosoma. Hilo linaimarisha uwezo wako na kujenga taswira kwenye akili yako, kitu unachoweza kutumia kuelewa vitu zaidi.
    6. Usomaji unakujengea uelewa zaidi. Kupitia usomaji, unaweza kuwaelewa wengine zaidi, unaweza kujiweka kwenye viatu vyao na kuwa na huruma kwa yale wanayopitia.

    Kuchukua hatua, naamini upo kama mimi rafiki yangu ambaye unapenda kujifunza vitu vipya kila siku. Kwa hivyo, ni wakati nzuri sasa wa kuamua na kuchukua hatua na kuanza kusoma hata kama ni kusoma kitabu kimoja kwa wiki, au kimoja wa mwezi kama unaanza kusoma vitabu.

    Akupendaye sana,

    Maureen Kemei.

    Mawasiliano:

    kemeimaureen7@gmail.com.

    Uamshobinafsi.com.

  • Sifa zinazowatofautisha wanaofanikiwa na wanaofeli.

    Rafiki yangu mpendwa kuna msemo unasema, there is nothing useless as doing efficiently that should not be done at all. Ikimaanisha kuwa hakuna kitu kisicho na maana kama kufanya kwa ufanisi jambo ambalo hukutakiwa kufanya kabisa.

    Ni kama kuandika majibu ya swali yasiyo yenyewe (O.P) – (Off Point).

    Wanaofanikiwa na wanaofeli hutofautiana kwenye kufanya au kutokufanya mambo haya mawili

    Mosi, Mambo mepesi na yasiyo muhimu.

    Hapa ndio watu wengi hutumia siku yao kwa masaa mengi. Watu wasiofanikiwa hupenda kufanya vitu vyepesi visivyo na umuhimu kama vile kutembelea mitandao ya kijamii, kupiga story na kadhalika wakati ana kazi ngumu   na za muhimu zinazotakiwa kufanyika lakini hazifanyi. Hivi ni vitu ambavyo haviongezi chochote kwenye mafanikio ya mtu, badala yake vinamkwamisha pasipo yeye kujijua.

    Mbili, Mambo magumu na ya muhimu.

    Haya ndio mambo yatakayokutofautisha na wengine kwa haraka, ni mambo yanayoleta mafanikio.

    Ni mambo kama kusoma vitabu, kujiendeleza kimaarifa, kuweka akiba, kuwekeza nk. Wana michezo wanatumia kanuni hii kufanya mazoezi mazito wanayowaongezea uwezo wakati wengine wamepumzika..
     

    Epuka mambo madogo madogo yanayokupotezea mwelekeo

    Kama unajua ni wapi unaelekea kimalengo ni lazima kila siku kujikagua na kuhakikisha upo kwenye uelekeo sahihi wa malengo yako.

    Epuka kabisa kwenda nje ya malengo yako hata kama ni kwa sekunde moja, kwa sababu mtu anayepotea kwa maili 1,500 huanza kupotea kwa sekunde.

    Hivyo hakikisha unajikagua mwelekeo wako kila mara.

    Mambo ambayo hutakiwi kuyavumilia kabisa ili usipoteze mwelekeo ni pamoja na haya yafuatayo:-

    Mosi, Kutojiingiza kwenye majukumu yasiyo ya lazima.

    Tunaishi katika ulimwengu wa social network (mitandao ya kijamii). Usipokuwa makini utajikuta kila mara unafanya vitu ambayo havina umuhimu kama kufuatilia habari, kuwafuatilia watu nk.

    Vitu hivyo haviongezi chochote kwenye mipango na malengo yako.

    Mbili, Kagua mtandao wa mahusiano yako.
    Watu unaohusiana nao kwa karibu wana nafasi kubwa ya kukuathiri, kukurudisha nyuma au kukusogeza mbele kimalengo.

    Ushawishi mdogo mdogo wanaotupatia unatosha kukuondoa kwenye misingi na njia ya mafanikio.

    Tatu, tambua tabia zinazoweza kupoteza mwelekeo wako.

    Kuna baadhi ya tabia kama unazo hata kama ungelikuwa mtu bora kiasi gani, anguko lako linakuwa lipo jirani.

    Tabia hizo ni kama vile, kupenda sana usingizi kuliko kawaida, uvivu wa kusoma, kushindwa kutunza ahadi zako, kutokuweka akiba, kutozingatia bajeti yako, kutokutunza siri, ulevi  na kutokupenda kazi.

    Kuchukua hatua ni wakati sasa rafiki yangu wa kuepuka tabia ambazo zinatuangusha na kujenga tabia zinazovuta mafanikio kwenye maisha yetu.

    Akupendaye sana.

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com

  • Sababu 2 za watu kushindwa kufanikiwa.


    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini kuna sababu kubwa mbili za watu kushindwa kufanikiwa kwenye mambo yao wanayoyapanga.

    Mosi, Ni kukosa Nidhamu (Indiscipline)

    Nidhamu ni uwezo wa kufanya jambo unalotakiwa kufanya bila kujali kama unajisikia kufanya au laa,

    Ni uwezo wa kufanya jambo muhimu bila usimamizi wala kuhimizwa na mtu yeyote yule.

    Ni hali ya kuwa na nguvu ya kila wakati  kufanya jambo lako muhimu bila kutoa visingizio.

    Kwenye maisha lazima ujiwekee nidhamu na uhakikishe unasimamia nidhamu hiyo; Kwa mfano nidhamu ya kusoma vitabu, nidhamu ya fedha, nidhamu ya kuamka mapema, nidhamu ya kutumia muda wa vizuri bila kupoteza nk

    Mbili, Kukosa nguvu ya mwendelezo (Inconsistance)

    Kufanya jambo kwa mwendelezo ni nguzo muhimu sana kwenye mafanikio yoyote.

    Hakuna namna unaweza kufanya jambo mara moja na kisha ukapata mafanikio mara hiyo moja.

    Mara nyingi, utahitaji kufanya jambo mara nyingi, utahitaji mfululizo wa kutenda. Utafanya utakwama na utapambana hadi mwisho utafaninikwa kukamilisha jambo hilo.

    Kuchukua hatua kwa ujumla rafiki yangu, bila mwendelezo wa kufanya jambo bila kuacha hakuna mafanikio. Na pia bila kuweka nidhamu kali ya kuamua na kufanya hakuna mafanikio.

    Akupendaye sana.

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Ni nini chanzo cha hofu.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini kuna hofu ya nje na ya ndani. Tumelelewa tangu utotoni na woga mwingi si kwa nje tu,bali pia kwa ndani.

    Hofu ya nje ni kama vile kupoteza kazi, kutokuwa na chakula cha kutosha, kupoteza nafasi yako, bosi wako kuwa na tabia inayo kuumiza.

    Hofu ya ndani ni kama hofu ya kutokuwa, hofu ya kutofanikiwa,hofu ya kifo,hofu ya upweke,hofu ya kutopendwa na hofu ya kuchoka kabisa.

    Chanzo kikubwa cha hofu ni utegemezi wa vitu,watu au mawazo huzaa hofu, utegemezi unatokana na ujinga,kutokana na ukosefu wa kujitambua, hutokana na umaskini wa ndani yaani wa fikra, hofu husababishwa kutokuwa na uhakika kiakili, huzuia mawasiliano na uelewa.

    Kupitia kujitambua tunaanza kugundua na hivyo kuelewa sababu ya hofu, sio tu ya juu juu lakini sababu kuu za hofu kwa ujumla.

    Hofu inapatikana au inatafutwa, inahusiana na wakati uliopita, na kwa hisia huru ya mawazo kutoka kwayo, wakati uliopita lazima utazamwe kwa jicho la sasa.

    Mambo yaliyopita yanataka kuzaa mambo ya sasa ambayo inakuwa kumbukumbu ya kutambua ubinafsi wako yaani ‘mimi’ na ‘vyangu’ . Ubinafsi ndio mzizi wa hofu yote.

    Kuchukua hatua, Ili kuondokana na hofu ya mambo yaliyopita ni bora kujitambua wewe ni nani ili litakusaidia kuepukana na mawazo yanayochangia hofu kwenye maisha yetu.

    Akupendaye sana.

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Mambo 10 ya kubadili leo hili kufikia mafanikio makubwa.

    Rafiki yangu mpendwa, kila mtu anataka mabadiliko, anataka maisha yake yawe bora, anataka kuwa na kazi au biashara mzuri, anataka kuwa na familia bora,anataka kuwa na uongozi mzuri na mengine mengi mazuri. Lakini linapokuja swala kwamba inabidi mtu abadilike ndio changamoto inapoanza.

    Kila mtu anataka aendelee kufanya kile ambacho amezoea kufanya, anataka kuendelea na maisha ambayo ameyazoea, lakini anataka kuona mabadiliko makubwa. Hii ni ndoto ya mchana ambayo haiwezi kutokea kwa njia yoyote ile.

    Rafiki yangu mabadiliko yanaanza na wewe na ndio vitu vingine vinabadilika, unabadilika kwanza wewe na ndio kazi yako, biashara yako,mwenza wako, watoto wako, wafanyakazi wako na jamii inayokuzunguka wanabadilika. Haiendi kinyume na hapo, kwamba hivyo vingine vyote vikishabadilika basi na wewe ndio utabadilika,hakuna kitu kama hicho.

    Kama unataka kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako? Haya ni mabadiliko kumi unayotakiwa kuyafanya sasa, kama imekuwa bado huyafanyi.

    Moja ni kuwa na matumizi mazuri ya muda wako,usiupoteze kwa mambo yasiyokuwa na msingi kwako.

    Pili ni usishiriki kwenye majungu,umbeya au kumsema mtu yeyote vibaya.

    Tatu weka juhudi kubwa sana kwenye kazi yako,nenda hatua ya ziada, fanya zaidi ya mtu mwingine yeyote.

    Nne acha matumizi mabovu ya fedha,nunua vitu ambavyo ni muhimu kwako.

    Tano acha kukaa na watu ambao wanakurudisha nyuma.

    Sita pata muda wa kukaa na familia yako na wale unaowapenda.

    Sapa usinunue kitu ili kuonekana,au kwenda na wakati.

    Nane kuwa mwaminifu,kuwa mwadilifu.

    Tisa timiza neno unaloahidi

    Kumi sema hapana mara nyingi uwezavyo jambo lolote ambalo halina manufaa kwako au halitakufikisha kwenye malengo yako sema hapana

    Kuchukua hatua,unajua hakuna mabadiliko yoyote ambayo yanaweza kutokea nje yako. Mabadiliko yoyote ya kweli yanaanza ndani yako mwenyewe rafiki yangu. Tunapaswa kuamua na kuchukua hatua ya kufanya mabadiliko kwenye maisha yako na wengine wanaokuzunguka bila shaka nao watabadilika.

    Akupendaye sana.

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@kemeimaureen

  • Sababu ya kuwa mwangalifu na wale wanaoonekana kuwa wema kwako.

    Rafiki yangu mpendwa pata picha kuna mtu unamwamini sana na kumtegemea kwa asilimia zote, kiasi kwamba huwezi ukafanya maamuzi bila ruhusa yake.

    Utajiskiaje kama mtu uyo anakuhadaa tu mwishowe anakutawala kwa sababu ulimpa nafasi ya kukutawala mwanzoni.

    Sina uhakika kama itakufaa, lakini kutoka kwenye kitabu cha the fountainhead by Ayn Rand, tunaona jinsi riwaya hii inavyotuonesha mwusika Ellisworth M.Toohey. Anaoneshwa kama mtu anayependa kuonekana ni mzuri mbele za watu Ili tu apate nafasi ya kuwatawala na kuwahandaa watu hao.

    Toohey alikuwa na sifa ya kuhakikisha watu hawafanyi kile wanachopenda, bali kile ambacho kinawasaidia wengine. Hasa pale anapogundua mtu anakipenda kitu sana,basi alimshauri asikifanyie kazi,hasa wakati wa mtu kuchagua asomee nini. Aliwaepusha sana vijana wasifuate kile wanachopenda, bali wafuate kile ambacho kitawasaidia watu. Aliamini mtu kusomea kile anachokipenda ni ubinafsi, na kusomea kile chenye manufaa kwa wengi ndiyo sahihi.

    Toohey aliwafanya wafuasi wake wamtegemee yeye,hivyo hawakuweza kufanya maamuzi bila yeye, na pia alikuwa akiwaambia kitu hawapingi,bali wanaiamini na kukifanya.

    Toohey aliendelea na falsafa yake ya kuwaweka wengine mbele kuliko maslahi yake mwenyewe. Kwa kufanya hivyo,aliweza kutengeneza wafuasi, ambao walimchukulia Toohey kama mtakatifu, mtu asiye na ubinafsi na kukosea.

    Aliamini kwamba ili mtu kufikia wema, mtu unapaswa kuweka maslahi ya wengine mbele kabla ya maslahi yake binafsi. Aliamini mtu hapaswi kujijali yeye mwenyewe kwa namna yoyote ile, bali kujali wengine kwanza. Kwa kifupi falsafa ya Toohey ilikuwa ni ya ujamaa, ambapo kundi ni bora kuliko mtu mmoja mmoja.

    Rafiki yangu tunayojifunza kwenye maisha ya Toohey ni kwamba, tunapaswa kuwa makini sana na wale wanaoonekana kuwa wema sana, lakini ndani ni mtu mbaya na mwenye nia ovu.

    Kitu kimoja zaidi tunapaswa kuepuka kumwamini mtu yeyote kiasi cha kumtuhusu atufanyie maamuzi muhimu ya maisha yetu. Hicho ni kitu ambacho kila mmoja wetu anapaswa kukifanya wenyewe. Kwa kwa kuwapa wengine ruhusa hiyo tutakuwa tumeruhusu atutawale. Kumbuka kwamba kila mtu ana ajenda zake kwa jambo lolote lile,japo nje ataonekana hana ajenda, lakini zipo.

    Kuchukua hatua, kama ambavyo tumejifunza hapa kwamba, tusiwape wengine ruhusa ya kufanya maamuzi kwa ajili yetu, tunapaswa kujiamini na kujisimamia kwenye kufanya maamuzi yetu sisi wenyewe, ili tuwe huru wa kufanya kile tunachokipenda bila kupingwa na yeyote yule.

    Akupendaye sana,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

    .

  • Sababu nzuri ya kusema hapana.

    Rafiki yangu mpendwa Ili uweze kusema hapana kwenye mambo yasiyo sahihi,lazima uwe na mambo sahihi unayosema ndiyo.

    Sina uhakika kama itakufaa, lakini lazima ndiyo yako iwe kubwa na muhimu kuliko hapana.

    Utajisikiajie kama utasema ndiyo kwenye mchakato unayofanyia kazi na sema hapana kwa mengine yote ambayo hayasaidii mchakato huo.

    Kitu kimoja zaidi ni kuwa ndiyo hapana zako zitawaumiza watu muda mfupi,lakini zitawasaidia kwa muda mrefu kupitia kile unachofanya, ambayo kwa kusema hapana kwenye mengine utakifanya kwa ubora sana.

    Lazima pia uwe na kiasi kwenye hapana zako,maana iwapo utasema hapana kwa kila kitu,itakuwa ni njia nyingine ya kujificha au unaweza kuwapoteza wale muhimu unaowahitaji sana kwenye kile unachofanya.

    Pata picha ulisema ndiyo kwenye mambo mengi nako unakosa muda na umakini wa kutosha kwenye kile muhimu unachofanya.

    Kuchukua hatua, kwa kuwa tumeona ndiyo yetu lazima iwe kubwa na muhimu kuliko hapana. Hivyo inatupasa tuweke vipaumbele vyetu kwa usahihi,tunasema ndiyo kwa yanayohusiana na vipaumbele vyetu na hapana kwa yasiyohusiana na vile vipaumbele vyetu.

    Habari njema rafiki yangu ni kuwa usiogope kuwaumiza watu kwa muda mfupi kwa hapana zako,kwani baadaye watanufaika na matokeo utakayozalisha.

    Akupendaye sana.

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.