-
Kwa nini unapaswa kujipa muda wa kufikiri na kutafakari.
Rafiki yangu mpendwa watu wengi hudhani kujibu haraka ni kuonekana una akili zaidi.
Yaani kwamba mtu anayechukua muda wa kufikiri kwa kina kabla hajajibu basi ni mjinga au hajui.
Sina uhakika kama itakufaa, lakini Derek kwenye kitabu chake cha ‘hell yeah or no’ anatuambia yeye ni mtu wa kufikiri kwa taratibu na huwa hakimbilii kujibu kitu chochote.
Huwa anajipa muda kwanza wa kukifikiri kwa kina na kujifunza kwa undani ndiyo aweze kujibu.
Anasema watu wanamuona ni mjinga kwa hilo, lakini inamsaidia kwa mengi. Linamwepusha na mabishano yasiyo na tija, lakini pia linamsaidia kujifunza vitu kwa kina.
Habari njema ni kwamba kufikiri kwa kina kunakusaidia uepuke kujibu haraka pale unapoulizwa chochote.
Utajiskiaje kama utakuwa unajipa muda wa kufikiri na kutafakari kwa kina kabla hujajibu mtu yeyote yule? Labda utajisikia vibaya lakini utakuwa umejipa muda wa kuangalia jambo kwa kina, hivyo basi kuepuka mabishano yasiyo na tija.
Kitendo tu cha kujipa muda kitakuepusha na mengi yasiyo na umuhimu kwenye maisha yako.
Rafiki yangu majibu mengi unayoyatoa kwa haraka huwa siyo sahihi, hata kama ni kitu ulichozoea, yanaweza kuwa na mabadiliko ambayo yalishatokea.
Hatua ya kuchukua; unapaswa kujipa muda kabla hujakimbilia kujibu chochote.
Na kama mtu anasisitiza ujibu haraka, jibu lako linapaswa kuwa sijui, au tutaona. Usiwe na wasiwasi maana hakuna ubaya wowote kwenye kutokujua.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
-
Jinsi hatua ndogo zinavyobadili utambulisho wako.
Rafiki yangu mpendwa unajua nini kuhusu kuchukua hatua ndogo ndogo kwenye kila siku yako?
Usiwe na wasiwasi maana kuna umuhimu mkubwa wa kuchukua hatua ndogo ndogo kwenye kila siku ya maisha yako.
Habari njema ni kwamba unapoanza kuchukua hatua ndogo kwenye kupambania ndoto zako inabadili sana utambulisho wako.
Pata picha unafikiria kufanya mambo makubwa na jinsi mambo hayo yatakavyokufanikisha kwenye maisha yako.
Rafiki yangu tunaposikia hadithi za wale waliofanikiwa tunaona walivyoanza na hatua ndogo ndogo.
Sina uhakika kama itakufaa, lakini watu hao waliofanikiwa walianzia hatua ndogo ndogo kama; kusema NDIYO pale mtu alipouliza watu wa kujitolea, kuwaendea wale waliofanikiwa, kusoma kitabu au hata kuchukua kozi fulani.
Rafiki kuna aina mbili za watu duniani, wale wanaochukua hatua ndogo ndogo kila siku na kufanya bila kuacha na wale wasiochukua hatua yoyote kabisa.
Habari njema ni kwamba unapokuwa umechukua hatua moja, unajiona kama shujaa na mbobezi kwenye kitu hicho.
Kabla hujafanya maamuzi, unapaswa kufanya kitu kimoja kinachokufanya ujione ni mkarimu na utaanza kuwa na ukarimu kwenye mambo mengine.
Kitu kimoja zaidi ni kufanya kitu kimoja kinachokufanya ujione ni kiongozi na utaanza kuwa kiongozi kwenye mambo mengine.
Hatua ya kuchukua; rafiki yangu dunia inakuchukulia vile unavyojichukulia wewe mwenyewe.
Matendo yako yanaidhihirisha dunia wewe ni mtu wa aina gani.
Kinachofuata baada ya hapa ni kuchukua hatua ndogo kabisa na hiyo itakubadili kabisa.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
-
Kitu pekee kinachodhihirisha thamani yetu.
Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini kitu pekee kinachodhihirisha thamani ni kuchukua hatua ya kufanya kuliko kuongea (yaani matendo na siyo maneno).
Unaweza kusema utakavyo, lakini watu wataamini zaidi kile unachofanya. Maneno ni rahisi, kila mtu anaweza kusema atakavyo. Lakini matendo ni magumu na hayo ndiyo yanayothihirisha kweli mtu anasimamia wapi.
Utajiskiaje kama kweli kitu ni muhimu kwako, alafu usikifanye, na ni kitu hicho unajua kabisa kuwa kingeleta mafanikio kwako? Lazima utajisikia vibaya, sio.
Lazima utakifanya kwa sababu hutaishia tu kusema. Kama unataka kitu kweli utafanya kila namna mpaka ukipate, hautakubali kuzuiwa na chochote. Hivyo, angalia yale unayofanya, hayo ndiyo yanaonyesha kuwa unajali zaidi.
Na hata kwa wengine, usisikilize wanasema nini, wewe angalia wanafanya nini. Kama maneno na matendo ya mtu vinatofautiana, amini zaidi matendo kuliko maneno.
Hivyo kitu kimoja zaidi ni kwa wale ambao kila mwaka wanasema wanataka kuanza biashara ila hawana mtaji, au uwezo, au muda au kingine chochote, jibu unalo hapo, hawataki kuanza biashara. Wengekuwa wanataka kweli wangeshaanza.
Kuchukua hatua; kinachofuata baada ya hapa ni kufanya maamuzi ya kufanya zaidi kuliko kuongea zaidi.
Rafiki yako.
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
-
Madhara ya kijilinganisha na wengine.
Sina uhakika kama itakufaa, lakini changamoto kubwa ya watu wengi kwenye zama hizi ni kijilinganisha na wengine.
Na kujilinganisha na wengine huwa na madhara ya aina mbili.
Moja ni pale mtu anapokuwa anajiona ana uwezo mkubwa kuliko wengine, hapo husukumwa kuthibitisha uwezo wao mkubwa na hivyo kuacha kujifunza.
Upande wa pili ni pale mtu anapojilinganisha na kuona wengine wana uwezo mkubwa kuliko yeye na hivyo kujidharau na kuona hawezi.
Tafiti pia zinaonyesha kuwa wenye kupenda kujilinganisha na wengine, huwa wakishindwa kwenye maisha wanatafuta wale walioshindwa zaidi yao ili kijilinganisha nao, kitu kinachowafanya wajiskie vizuri.
Badala ya kuangalia wale waliofanikiwa kuliko wao na wajifunze kwao, wao wanataka walioshindwa zaidi, lengo siyo kujifunza, bali kujisikia vizuri, kwa sababu wanaamini uwezo wao una ukomo.
Kuchukua hatua; kinachofuata baada ya hapa rafiki, ni kuacha kujilinganisha na wengine, lakini habari njema ni kuwa una uwezo mkubwa sana ndani yako ambayo itakusaidia sana uishi kusudi lako na hivyo basi, utaacha kujilinganisha na wengine.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
uamshobinafsi.com.
-
Imani za kujijengea ili usijiwekee ukomo.
Tambua kwamba huwezi kupata muda, bali unapaswa kutenga muda. Kama kitu ni muhimu, unatenga muda wa kukifanya . Hapa unahitaji kuweka vipaumbele vyako sawa.
Tambua ukweli huu kwamba hulazimiki kufanya chochote kile. Kila unachofanya na muda wako, umechagua mwenyewe. Hakuna aliyekushikilia bastola na kukuambia usipofanya hivi nakuua. Umechagua mwenyewe hivyo mamlaka ni yako, unaweza kuchagua kwa namna nyingine kama ulivyochagua sasa haikuridhishi.
Pima matumizi yako ya muda kwa sasa. Chukua siku saba na orodhesha yote unayofanya kwenye muda wako. Zoezi hilo litakuonyesha wapi muda wako unapotelea zaidi na hivyo kuweza kuuokoa.
Lenga kupata masaa mawili huru kila siku. Baada ya kuorodhesha yote unayofanya kwenye siku yako, angalia ni yapi ambayo hayana tija na yafute. Lengo ni uweze kupata angalau masaa mawili kila siku, ambayo unaweza kuyatumia kwa yale muhimu unayochagua.
Kwa nini masaa mawili? Moja kwa kuwa itakusukuma kuondoa ukomo ulionao. Na mbili kwa sababu ukiyawekeza vizuri masaa hayo mawili kila siku, utaweza kufanya makubwa.
Tambua kila ndiyo ni hapana . Unaposema ndiyo kwenye jambo moja, maana yake unasema hapana kwenye jambo jingine . Kwa kuwa na masaa 24 tu kwa siku, lazima uchague kwa umakini mambo gani yakusema ndiyo na yapi yakusema hapana.
Ondoka kwenye mazoea. Kinachofanya ukose muda ni mazoea ambayo tayari umeshajijengea .Kuna aina ya maisha umeshayajenga kwako ambapo kuna vitu unafanya kama sehemu ya maisha yako.Ni wakati wa kuyamulika maisha yako na kuvunja kila mazoea yanayokupozea muda. Hili halitakuwa rahisi maana litaathiri wengine, lakini lazima ulisimamie.
Kupata muda zaidi, fanya haya; acha kuangalia tv, kusoma magazeti, na kuzurura kwenye mitandao ya kijamii.
Tenga muda wa kujibu simu, jumbe na barua pepe, usiruhusu hivyo kuwa usumbufu kwako muda wote.
Andaa na kula vyakula bora kwa afya yako. Hilo litapunguza muda na uchovu.
Jilazimishe kupata muda. Kama bado unaona huwezi kupata muda, jua ni ukomo tu unakuambia hivyo na siyo ukweli.
Pata picha umeumwa sana, ukaanguka na kupoteza fahamu, ukapelekwa hospitali na kulazwa kwa wiki nzima.
Baada ya vipimo mbalimbali, daktari anakuambia una ugonjwa ambao tiba yake pekee ni kila siku utenge masaa mawili ya kukaa kwa utulivu bila ya kufanya chochote.
Na kama siku itapita hujatenga masaa hayo mawili, utaumwa na kuzimia tena na ukizimia mara ya pili uwezekano wa kufa ni mkubwa.
Sasa niambie, hutayapata masaa mawili kwa siku? Jibu liko wazi, utayapata tu. Hivyo muda upo, ni wewe kujisukuma uweze kuutenga na kuutumia vizuri.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
-
Namna ya kudhibiti fikra zako.
Rafiki yangu mpendwa watu wengi hudhani hawawezi kudhibiti fikra zao. Lakini hilo siyo kweli, kudhibiti akili na fikra ni kitu kinachowezekana kabisa.
Na kwa kuwa akili zetu ndiyo zinatupa kila kitu kwenye maisha yetu, udhibiti wake ni hatua muhimu ambayo kila mtu anapaswa kuifanyia kazi.
Kudhibiti akili na fikra ni kitu ambacho kimekuwa kinafundishwa tangu enzi na enzi, kuonyesha ni jinsi gani jambo hilo lina umuhimu mkubwa.
Watu wengi wanalalamika kwamba hawawezi kuweka umakini wao kwenye kitu kimoja. Lakini ukweli ni kwamba nguvu iyo ipo kwa kila mmoja, kinachohitajika ni kuendeleza.
Kudhibiti fikra ni hatua muhimu kwenye kudhibiti maisha. Bila ya kudhibiti akili hakuna kingine kikubwa kitakachowezekana. Na kutokana na umuhimu huo, zoezi la kwanza kwenye siku linapaswa kuwa kudhibiti akili.
Huwa tunaweka juhudi kubwa kwenye kutunza miili yetu, kuanzia kuilisha, kusafisha na kuivalisha. Lakini hakuna juhudi tunaweka kwenye akili, ambayo ni muhimu sana.
Hivyo basi, ule muda wa asubuhi ambao unatoka nyumbani kwenda kwenye shughuli zako ndio unapaswa kuutumia kufanya zoezi la kudhibiti akili.
Kazi yako ni kuhakikisha mawazo yako yanakaa kwenye kitu kimoja ulichochagua. Yatahama mara kwa mara, lakini yarudishe kwenye kile ulichochagua.
Kama unajiambia akili yako haiwezi kuweka umakini kwenye kitu kimoja, kumbuka siku ulipewa jukumu kubwa na linalohitajika haraka.
Akili yako ilitulia kwenye jambo hilo bila kuhama. Hicho ni kiashiria kwamba huo uwezo unao, ni wewe kuufanya kazi kwa makusudi ili kuimarisha umakini wako.
Kuchukua hatua kwa namna yoyote ile usiache tu akili yako izurure hovyo, badala yake idhibiti kwa kuweka mawazo yako kwenye kitu kimoja kwa muda mrefu.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
-
Jinsi ya kubali yaliyo nje ya uwezo wetu.
Rafiki yangu mpendwa kwenye falsafa ya ustoa, kuna dhana moja ambayo inaitwa amori fati ikiwa na maana kwamba, ipende hatima yako yaani love your fate.
Maana ya kubwa ya dhana hii kwenye falsafa ya ustoa ni kwamba wastoa waliamini tunapaswa kupokea kila kitu kinachotokea kama vile tulitaka kitokee.
Hii ina maana kwamba, chochote kile kinachotokea, kwanza unakipokea na kukikubali kisha unachukua hatua kuhakikisha kinakuwa na manufaa kwako.
Kukataa kukubali na kupokea yale yaliyo nje ya uwezo wako ni kukubali kuumizwa zaidi na pia ni kuchagua kuwa kiranja wa dunia. Kuwa kiranja wa dunia ni kazi kubwa na ipo nje ya uwezo wa binadamu kabisa.
Kwa kukubali yale yaliyo nje ya uwezo wako unajipa nafasi ya kuweza kuyavuka yasiwe kikwazo kwa mafanikio yako.
Sina uhakika kama itakufaa, lakini kwenye falsafa ya ustoa kuna upacha wa kila kitu, kama kuna mazuri basi unapaswa kujua kuwa kuna mabaya pia. Pale leo unapopitia na kufurahia mazuri jua kuwa kuna siku utakuja kupitia mabaya pia.
Kupenda hatima yako ni kukabiliana na yote ambayo asili imeamua juu yako na wala siyo kulalamika.
Kwenye maisha maumivu huwa hayakosekani, kuna mambo mengi huwa yanakwenda kinyume na matarajio yetu.
Lakini mateso ni kitu ambacho mtu unajichagulia mwenyewe. Unachagua mateso pale unapojaribu kukataa kile kinacholeta maumivu (yaani kujaribu kuwa kiranja wa dunia).
Ukikubali kile kinacholeta maumivu unaacha kuteseka na kuona hatua zipi sahihi za kuchukua. Kwa kila unalokutana nalo kwenye maisha yako linaweza kuwa ndani ya uwezo wako kudhibiti au nje ya uwezo wako.
Kuchukua hatua; rafiki yangu kwa yaliyo ndani ya uwezo wako chukua hatua sahihi katika kukabiliana nayo. Na usikubali kilicho nje ya uwezo wako kuwa kikwazo kwako, kikubali kisha kivuke Ili uweze kufanikiwa.
Kitu kimoja zaidi ni kwamba kamwe usikubali kuwa kiranja wa dunia, kwani huko ni kukubali kujiumiza kwa kutaka kufanya yaliyo nje ya uwezo wako.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
uamshobianfsi.com.
-
Umuhimu Wa Wewe Kuwa Tajiri.
Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini kinachowatofautisha wanaotajirika na wanaobaki masikini ni tabia.
Hivyo kwa kuzijua tabia za kitajiri na kuziishi kwenye maisha yako ya kila siku, unakuwa kwenye nafasi nzuri ya kufikia utajiri pia.
Mambo mengi sana yamekuwa yanasemwa kuhusu utajiri na matajiri, lakini mengi kati ya mambo hayo siyo sahihi. Mengi yanasemwa kuhusu utajiri na matajiri, hasa kwa upande hasi siyo sahihi na yamewafanya wengi kuendelea kubaki kwenye umasikini.
Ukweli ni kwamba utajiri ni mzuri, pale mtu unapoweza kuwa na fedha unazohitaji kwa ajili ya mahitaji ya maisha yako. Na pale unapokosa fedha, maisha yanakuwa siyo bora, kuanzia kwako binafsi na hata kwenye mahusiano yako.
Hivyo yeyote anayesema utajiri siyo muhimu, anajidanganya tu na kujipa moyo. Fedha na utajiri ni vitu muhimu sana kwenye maisha yetu ya kila siku.
Ukweli wa kuumiza ni kwamba katika kila jamii, yaani ukianza na dunia nzima, ukaja kwenye nchi ukaenda kwenye mkoa, wilaya na hata mtaa, utajiri umegawanyika kwenye namba ambazo ni sawa kwenye kila eneo. Namba hizo ni 99/1,95/5 na 90/10.
Namba ya kwanza ni 99 kwa 1, ikimaanisha asilimia 1 ya watu kwenye eneo ndiyo wenye utajiri mkubwa mno duniani, kushinda asilimia 99 kwa ujumla. Hii ina maana katika watu 100, mmoja ana utajiri mkubwa kushinda jumla ya utajiri wa wale wengine tisini na tisa.
Namba ya pili ni 95/5 ikimaanisha asilimia 5 ya watu kwenye eneo ndiyo wanaokuwa na utajiri na uhuru wa kifedha, huku asilimia 95 wakiwa na maisha ya kawaida au ya chini kabisa. Wale waliopo kwenye asilimia 5 hata kama siyo matajiri kama asilimia moja, lakini maisha yao yana ya uhuru mkubwa. Hawa hutawaona kwenye orodha ya matajiri wakubwa, lakini wameshafikia uhuru wa kifedha na wanaishi maisha bora sana kwao.
Namba ya tatu ni 90 kwa 10, ambapo asilimia 10 ya watu wanakuwa na utajiri au maisha ya juu, huku asilimia 90 ya watu wakiwa na maisha magumu sana. Hii ina maana katika watu 100, watu 90 wapo kwenye hali ngumu sana kifedha, hawana uhakika kesho au mwezi ujao wanaendeshaje maisha yao. Hawa ni watu ambao kila wakati wanaishi kwa wasiwasi kwa sababu hawana msingi wowote kifedha.
Namba sahihi kwa wewe kuwa ni kwenye 95/5 unapaswa kuwa kwenye asilimia 5 ya juu kwenye jamii yako na hata dunia kwa ujumla kwa kuwa na uhuru wa kifedha, kuwa na fedha ambazo unaweza kuendesha maisha yako kwa namna unavyotaka wewe.
Hii ni namba sahihi kwako kwa sababu hujitaji kushindana na yeyote na wala hujitaji kuwa na bahati kuifikia. Kwa kujijengea tabia nzuri, kuweka juhudi kubwa na kutokukata tamaa, utaweza kufika kwenye asilimia 5 ya juu na maisha yako yakawa bora sana.
Kabla hujafanya maamuzi napenda kukushirikisha kauli ambayo Kocha Dr Amani Makirita huwa anasema kuwa, utajiri ni mchezo, mchezo ambao una kanuni zake na sheria zake. Na ili uweze kushinda mchezo huu, lazima uzijue kanuni na uzishike sheria.
Wengi wamekuwa wanaingia kwenye mchezo wa utajiri kama vile ni kitu cha kubahatisha, hawajui kanuni wala sheria, hawana maandalizi na kinachotokea ni kushindwa vibaya sana.
Kuchukua hatua, rafiki yangu tuna kazi kubwa ya kufanya, kuhakikisha kuwa tunapambana ili tuifikie namba sahihi ya utajiri ya 95/5. Kwa sababu tunakuwa tunajijengea tabia nzuri ya kuweka juhudi kubwa kwenye kazi na biashara zetu, na pia kuweza kuwekeza kwa namna sahihi bila kukata tamaa. Na bila shaka tutafikia utajiri na uhuru wa kifedha na kuweza kufanya mambo yetu kwenye maisha yetu.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
-
Tatizo la kukata tamaa.
Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini je, unatumia muda mwingi kufikiria kuwa wewe huyuko mzuri sana kwenye kuchukua hatua ili kufikia malengo yako.
Aina kama hizi za mawazo zinakuzuia kwenye kuifikia malengo yako . Ukikata tamaa mapema, utakaso fursa nzuri kwenye maisha yako. Kuanguka ni nafasi nzuri kwenye maisha kama tu utasonga mbele na kama utajifunza Ili usirudie kosa hilo.
Ni ngumu kufanikiwa bila kukosea hata kwa mara moja, chukua mfano wa Theoder Geisel ambaye anaitwa pia Dr. Seuss ambacho kitabu chake cha kwanza kilikataliwa na zaidi ya wachapaji ishirini.
Baadaye aliweza kuchapa vitabu 46 ambavyo vinajulikana kama vitabu vya watoto, zingine zimebadilishwa kama film za tv, feature film na Broadway musicals.
Kama angekata tamaa hangepata dili ya kuchapa vitabu vyake, dunia haingekuja kutambua kazi yake ya uandishi ambayo yamekuwa ya kipekee na yamewafurahisha watoto kwa miaka.
Kukata tamaa baada ya anguko moja inaweza kufanya mtu atosheke vivyo hivyo. Wakati wote unaona haija haja ya kuendelea na mapambano, unaona kuwa kuanguka ni mbaya, kutakufanya usiendelee kujaribu tena. Hivyo kuogopa kwako kuanguka ndipo kutakuzuia usijifunze zaidi.
Mnamo mwaka1998 uchapaji wa the journal of personality and social psychology, watafiti walilinganisha watoto wa chekechea ambao wanapongezwa kwa akili zao na wale wanaopongezwa kwa jitihada zao.
Watoto wote walipewa mtihani ngumu, walipopewa matokeo yao walipewa chaguo mbili; waangalie matokeo ya wale waliofeli au waangalie matokeo ya wale waliopita.
Watoto waliokuwa wamezoea kupewa pongezi kwa sababu ya akili zao wote walikuwa wanataka kuona matokeo ya wale waliofeli ili waonekane wao ndio wanaweza
Lakini watoto waliokuwa wanapongezwa kwa sababu ya jitihada zao walikuwa tayari kujifunza kupitia matokeo ya wale waliopita ili warekebishe makosa yao.
Kama unaogopa kufeli, hutakuwa tayari kujifunza kupitia makosa unayofanya, hivyo hutathubutu kujaribu tena.
Rafiki yajo,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
http://www.uamshobinafsi.com/
-
Zawadi Yenye Thamani Kubwa.
Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini kitu kigumu zaidi kurudisha kwenye maisha ni muda uliopotea. Ukishapoteza muda, huwezi tena kuupata.
Muda ni zawadi yenye thamani kubwa, kwa sababu ni kupitia muda ndiyo tunaweza kufanya yote tunayopanga kufanya.
Lakini wapo maadui wawili ambao wamekuwa wakiiba na kupoteza muda wa wengi. Maadui hao ni uvivu na kuhairisha. Uvivu ni kutokuweka juhudi za kutosha kwenye kile unachofanya. Na kuahirisha ni kutokufanya kabisa, kuendelea kusogeza mbele yale unayopaswa kufanya.
Kama huweki juhudi za kutosha kwenye kitu unachokifanya, unaopoteza muda unaoweka kwenye kitu hicho. Na kama unahaairisha kufanya yale ambayo ni muhimu, unajua kabisa muda hausubiri wala kurudi nyuma.
Ubaya wa muda ni kwamba utaendelea kwenda, iwe unafanya yaliyo sahihi au la. Hakuna namna muda utasimama kukusubiri wewe mpaka uwe tayari. Hivyo kinachohitajika ni wewe kutumia vizuri muda ulionao, kwani ndiyo kitu pekee kinachokutofautisha na wengine.
Huwa kuna usemi kuwa muda ni pesa, lakini ni zaidi ya hapo, muda ni zaidi ya pesa, muda ni mfalme. Ukipoteza fedha unaweza kupata nyingine, ukipoteza muda huwezi kupata tena mwingine. Ndiyo maana unapaswa kupangilia na kuilinda sana muda wako wa kila siku ili uweze kuutumia vizuri kufanya makubwa.
Joe Girard kwenye (13 Essential Rules Of Selling) anatushauri kuwa tunapaswa kuelewa thamani ya muda wetu, kuupangilia vizuri muda huo na kufuata kila mpango wetu bila ya kuruhusu chochote kile kituyumbishe. Kwa kuwa na mipango unayoifanyia kazi,muda unakuwa rafiki yako mzuri na siyo adui kama wengi wanavyokuwa wanachukulia.
Kwa kuupangilia muda wako vizuri hutapoteza kwenye vitu visivyokuwa na tija. Pangilia mambo yako kwa namna ambayo unakuwa na kila unachokihitaji kwa wakati husika badala ya kupoteza muda kutafuta au kusubiri kitu pale unapokuwa unakihitaji..
Siyo lazima mipango yako iwe na ukamilifu, bali unapaswa kuwa sehemu ya kuanzia kukuongoza kwenye yale unayotaka.
Kuchukua hatua; rafiki yangu sehemu ya mipango unayokuwa nayo ni kuendelea kujifunza kuhusu kile unachofanya ili kuzidi kuwa bora kwenye kukifanya.
Habari njema ni kuwa kujifunza ni kutumia vizuri muda wako ili kuweza kufanya makubwa zaidi.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.