Home

  • Sababu Nzuri Ya Kusema Hapana.

    Rafiki yangu mpendwa naamini upo kama unapenda kuwa chanya mara zote kwa kufanya yale yanayochangia uchanya kwenye maisha yako.

    Ili uweze kusema hapana kwenye mambo yasiyo sahihi kwenye maisha yako, lazima uwe una mambo sahihi unayosema ndiyo.

    Lazima ndiyo yako iwe kubwa na muhimu kuliko hapana. Sema ndiyo kwenye mchakato unaofanyia kazi na sema hapana kwa mengine yote ambayo hayasaidii mchakato huo.

    Ndio, hapana zako zitawaumiza watu kwa muda mfupi, lakini zitawasaidia kwa muda mrefu kupitia kile unachofanya, ambapo kwa kusema hapana kwenye mengine utakifanya kwa ubora sana.

    Lazima pia uwe na kiasi kwenye hapana zako, maana iwapo utasema hapana kwa kila kitu, itakuwa ni njia nyingine ya kujificha au unaweza kuwapoteza wale muhimu unaowahitaji sana kwenye kile unachofanya.

    Ukisema ndiyo kwenye mambo mengi nako unakosa muda na umakini wa kutosha kwenye kile muhimu unachofanya.

    Chukua hatua, rafiki yangu weka vipaumbele vyako kwa usahihi, sema ndiyo kwa yanayohusiana na vipaumbele vyako na hapana kwa yasiyohusiana.

    Habari njema ni kwamba usiogope kuwaumiza watu kwa muda mfupi kwa hapana zako, kwani baadaye watanufaika na matokeo utakayozalisha.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Jinsi Ya Kutokuwa wa Kawaida.

    Rafiki yangu mpendwa, jamii huwa inapenda tuwe wa kawaida ili iwe rahisi kutudhibiti. Hivyo pale unapoenda tofauti na jamii inavyotaka uwe, unaonekana kama mtu wa ajabu na aliyepotea. Lakini hiyo ndiyo njia pekee ya kufanya makubwa na kufanikiwa.

    Huwezi kufanikiwa kwa kufanya yale yaliyozoeleka na kuwa kama wengine wanavyotaka uwe. Utafanikiwa kwa kujisikiliza mwenyewe, kutambua utofauti wako na kuuishi. Usijiskie vibaya pale unapokuwa tofauti na wengine. Jua huo utofauti wako utakaokufikisha kwenye mafanikio makubwa, kama utaweza kuutumia vizuri.

    Unapoujua utofauti wako usiufiche wala kujionea aibu, badala yake uishi kwa kujivunia. Hata kama watu hawakuelewi, wewe ishi huo utofauti wako na waache wayaone matokeo ya tofauti unayozalisha kupitia utofauti wako.

    Jamii inapenda kuwaweka watu kwenye makundi ya kazi ambayo yanaeleweka . Hivyo itakulazimisha pia ujitambulishe kwa kundi fulani linaloeleweka. Kama wewe unaona hakuna kundi moja linalokufaa, usijilazimishe kuingia kwenye kundi lolote. Wewe tengeneza kundi lako linalokufaa, linaloendana na utofauti wako.

    Jamii inapenda kuwaambia watu wabobee kwenye kitu kimoja. Kama hilo lipo ndani yako fanya hivyo. Lakini ndani yako unasukumwa kufanya kitu zaidi ya kimoja, fanya. Muhimu ni kutokuzima moto mkubwa unaowaka ndani yako, kwani huo una nguvu ya kukuwezesha kufanya makubwa.

    Ukweli ni hakuna mtu yeyote anayekujua wewe na uwezo mkubwa ulio ndani yako. Wakati mwingine hata wewe mwenyewe hujijui vizuri, kwa sababu umekuwa unahangaika na mengi na kujisahau wewe mwenyewe.

    Chukua hatua, rafiki yafanye maisha yako kuwa safari ya kujitambua, kujisikiliza na kupambana kuwa bora kadiri unayokwenda. Kwa kufanya hivyo, utaweza kufanya makubwa na ya tofauti kabisa na yale wanayofanya wengine.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com

  • Kama Unataka Kufanikiwa Basi Jenga Urafiki Na Mtu Huyu.

    Rafiki yangu mpendwa huwa tunakatishwa tamaa kutokana na kuwaambia watu ndoto zetu ambao hawafanani na sisi kimaono na hata kimtazamo kabisa.

    Kwa mfano ukienda kuomba mtu ushauri mtu aliyekata tamaa ya maisha sidhani kama utapata tumaini la maisha kutoka kwake.

    Kuna watu ukienda kuongea nao unajihisi tayari wewe ni mwanamafanikio lakini kama kuna wengine ukiongea nao wanakutoa katika hamasa ya mafanikio kabisa.

    Nani unayemwambia ndoto zako? Mtu hasi au chanya? Kumwambia mtu hasi ndoto zako ni mwanzo wa kujichimbia kaburi wakati bado uko mzima.

    Huwa tunakuwa na ndoto kubwa kweli, tunapenda kufanya mambo makubwa na tunakuwa na hamasa lakini tunawaambia watu ambao siyo sahihi katika ndoto zetu huwa tunajiharibia wenyewe.

    Watu hasi huwa wanazima ndoto za watu wengi kama vile mshumaa unavyopotea .

    Rafiki, kama umekosa watu chanya wa kuambatana nao katika jamii yako, wako marafiki chanya siku hizi unaweza kutembea nao ambao ni kama vile vitabu, watu chanya waliofanikiwa, kuliko kupoteza muda na watu hasi tumia muda wako kusoma vitabu utakuwa chanya.

    Haijalishi watu wanasema nini, lakini wewe ndiyo unatakiwa kuwa chanya zaidi ya wengine wote katika kile unachoamini.

    Wewe ndiyo dereva wa maisha yako unajua wapi unataka kwenda usikubali mtu aje akurudishe nyuma na kukupitisha njia ambayo siyo kabisa. Una maamuzi ya kuamua vile unavyotaka usiwaruhusu watu wakuamulie sana maisha yako wakati wewe mwenyewe bado uko hai.

    Ukiwa umekufa basi unakuwa huna thamani na huna kauli ya kusema ufanyiwe vipi na maiti haina haki. Sasa wewe uko hai kubali kutetea haki zako usikubali uwe maiti wakati uko hai.

    Hatua ya kuchukua, uwe na msimamo mkali juu ya maisha yako. Watu wakujue kabisa wewe ni mtu wa namna gani.

    Usiwe ni mtu wa ndiyo kwa kila mtu badala yake kuwa mtu wa hapana na ukiamua kufanya kitu fanya kweli na washangazwe watu kwa matokeo bora. Chochote kinachopita kwenye mkono wako acha alama isiyofutika.

    Mwandishi,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Je, Unajua Upo Hata Duniani Kwa Kusudi?

    Rafiki yangu mpendwa kuna umuhimu wa wewe kujua kwamba upo hapa duniani kwa kusudi maalum.

    Nadhani bado hujaweza kujua lakini haupo hapa duniani kwa ajali au bahati mbaya. Bali upo hapa duniani kwa kusudi maalum.

    Habari njema ni kuwa kuna kitu wewe unaweza kufanya ambacho hakuna mwingine amewahi kufanya au atakuja kufanya. Maisha yako ni tukio la mara moja tu duniani, tukio ambalo halitakuja kujirudia tena.

    Jua kusudi la uwepo wako hapa duniani na uliishi hilo, ndiyo njia pakee ya kuweza kufikia ndoto kubwa ulizonazo.

    Una uwezo, vipaji, mtazamo na zawadi za kipeke, vitu ambavyo haviwezi kupatikana kwa wengine kama vinavyopatikana kwako. Vitumie hivyo kwenye kile unachofanya.

    Umezaliwa na nguvu za kipekee kabisa za kuweza kuleta mabadiliko kwenye maisha yako na ya wengine pia.

    Rafiki yangu usipoteze nguvu hizo kwa kuhangaika na yasiyo na tija, bali zitumie vizuri ili uweze kuleta mabadiliko ya kweli na yenye tija.

    Chukua hatua; rafiki unajua unataka na unaweza kufanya makubwa zaidi ndiyo maana unasoma makala hayo. Amini zaidi kwenye hilo na chukua hatua kufanya makubwa.

    Mwandishi,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Nguvu Kuu Ya Kukataa Kukataliwa.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa lakini kama unataka uwe na nguvu kubwa ya kuweza kukataa kila unachokataliwa.

    Kama unataka uweze kuvuka kila aina ya ukatishaji tamaa na ukosoaji.

    Unapaswa kuunganisha ndoto yako kubwa na kitu ambacho ni kikubwa kuliko wewe.

    Unapoweka ndoto kwa ajili yako tu, ni rahisi kukata tamaa pale unapokutana na magumu.

    lakini ndoto yako inapohusisha watu wengine, unapata nguvu ya kukipambania zaidi kwa sababu unajua ikishindwa siyo wewe tu unayeathirika, bali na wengine pia.

    Kuwa na kusudi kubwa la maisha yako, kusudi linalokupa wajibu mkubwa na wajibu huo unakusumbua uendelee kupambana hata pale mambo yanapokuwa magumu.

    Kipimo cha mafanikio ya kweli kwenye maisha yetu siyo kile ambacho tumeweza kupata, bali jinsi ambavyo tumegusa maisha ya wengine kupitia kile tunachokifanya.

    Chukua hatua ; kwa kuangalia nini wengine wananufaika kupitia unachokifanya, unapaswa ulipe hilo kipaumbele, usiangalie tu ni nini unapata, bali pia angalia ni nini unatoa kwa wengine.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Njia 5 za kukabili ukosoaji.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini pale mtu anapotoa ukosoaji wa kukukatisha tamaa, usikubaliane naye kama ndiyo ukweli. Muone kama mtu anayeleta uchafu ndani kwako.

    Njia ya kwanza ni kwenye kila ukosoaji, angalia kipi ni kweli na unachoweza kutumia kuboresha kile unachofanya. Tumia hicho na puuza vingine vyote. Hapo jiulize maswali kipi ni kweli kwenye hii? Kipi naweza kutumia kuboresha na kukuza zaidi ninachofanya? Kwa kujibu maswali hayo, utaona kama kuna mazuri ya kutumia.

    Angalia chanzo cha ukosoaji, mwangalie yule anayekukosoa na jiulize kama ni mtu unayemheshimu na anayejua unachofanya. Watu wanaoelewa kile unachofanya huwa hawatoi ukosoaji wa kukatisha tamaa. Ukosoaji wao huwa ni wa kujenga zaidi. Hivyo unapojua yule anayekukosoa, unajua kama upokee au upuuze.

    Waonee huruma wakosoaji wanaokukatisha tamaa. Wengi wao ni watu wasio na ndoto kubwa na wasioamini makubwa yanawezekana.

    Ndiyo maana wana muda mwingi mpaka wa kuwakatisha tamaa wengine. Baada ya kuumizwa na watu hao, waonee huruma, waonee huruma jinsi ambavyo hawana makubwa ya kufanya kwenye maisha yao mpaka wanakatisha wengine tamaa, ni maisha magumu sana hayo.

    Cheka . Kwa ukosoaji wa wengi ambao wanakukatisha tamaa, ishia tu kucheka, hasa pale wanapokuambia mambo unayojua siyo kweli. Usibishane nao wala kutaka kuwaelewesha, wewe cheka tu.

    Usimjibu mtu yeyote ukiwa na hasira, hisia kali au umelewa. Katika nyakati hizo unakuwa hufikiri vizuri, hivyo jizuie kujibu.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Kukosolewa ni sehemu ya maisha.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini pale unapofanya kitu chochote cha tofauti na cha kibunifu, moja kwa moja unakuwa umekaribisha wakosoaji.

    Rafiki yangu, nadhani bado hujaweza kuelewa kuwa kukosolewa ni sehemu ya maisha ya kila siku.

    Yaani kila siku kuna watu wanakukosoa kwa namna mbalimbali. Unavyovaa, unavyofanya kazi zako, unavyoishi maisha yako.

    Watu unaokutana nao njiani na wasiokujua kwa namna yoyote ile wanakuhukumu. Watu wako wa karibu pia wanakuhukumu. Watu unaokutana nao mitandaoni wasiojua chochote kuhusu wewe pia wanakuhukumu.

    Hata wewe mwenyewe kuna wakati huwa unajihukumu kwa yale unayofanya. Na pia umekuwa unawahukumu watu wengine hata usiowajua kwa undani. Kuhukumu ni sehemu ya maisha ya wanadamu.

    Hivyo usiumie pale unapohukumiwa au kukosolewa, badala yake jua upo ukosoaji mzuri kwenye manufaa kwako na upi siyo mzuri unaopaswa kuupuuza.

    Tambua kila kitu unachokipenda na kukikubali kwenye maisha, kuna wengine ambao hawakupendi hawakukubali.

    Kuwepo kwa watu wanaochukia kile unachopata haimaanishi ni kitu kibaya, bali ni wao hawawezi kukielewa.

    Kile ambacho wengi wanasema ni ukosoaji, siyo ukosoaji kweli, bali ni maoni yao kuhusu kitu fulani.

    Tatizo la maoni kila mtu ana yake na huwa yanachochewa zaidi na hisia hivyo hayawi sahihi.

    Mtu anapokosoa kitu kwa sababu hakipendi au hakielewi, ukosoaji wake hauwezi kuwa sahihi, hayo ni maoni yake, ambayo siyo ukweli.

    Chukua hatua; tambua kwamba chochote unachofanya siyo kwa ajili ya kila mtu, bali kwa ajili ya watu wa aina fulani ambao unajua jinsi ya kuwafikia.

    Unapochagua wale unaowalenga, unawaandalia kile chenye manufaa kwao na kuwapuuza wengine.

    Watu hao wanapokupa maoni yao, yanakuwa na manufaa kwako kwa sababu yanaendana na kile unachofanya.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Jinsi ya kukataa kukataliwa.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini kuamini kwamba kila kitu kinawezekana hakumaanishi kila wakati utapata kile unachotaka.

    Utakutana na watu wengi watakaokupinga na kukukatalia, watakaokuambia huwezi na haiwezekani.

    Ikiwa kweli unakadiria kupata unachotaka, basi lazima ukatae kukataliwa.

    Watu wanapokukatalia usikubaliane nao, wewe kataa na amini kile unachotaka kinawezekana na kuwa ta tayari kukipambania.

    Hutapata ushindi mara zote, lakini njia pekee ya kujua nini hasa unachoweza kufanya ni kujaribu makubwa ambayo hujawahi kufanya.

    Jenga tabia ya kuhoji kila sheria na kila ukomo ambao umeweka. Jiulize kama ni kweli au ni mazoea tu ambayo watu wanayo.

    Kabla hujafanya maamuzi, unapaswa ujaribu mwenyewe kile unachoambiwa hakiwezekani badala ya kuamini tu unachoambiwa.

    Na habari njema ni kwamba ni kupitia kufanya ndiyo utajifunza mengi juu ya uwezo wako, utaweza kufanya yanayowashangaza wengi.

    Chukua hatua; rafiki yangu yote unayofikiria kuyafanya yatawezekana tu kama utaanza na imani kwamba kila kitu kinawezekana na kukataa kukataliwa.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Unajua unachagua kuwa na furaha.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini furaha, upendo na hamasa siyo vitu unavyotafuta, bali ni machaguo unayofanya.

    Akili zetu ni kitu unachochagua na ujuzi unaojijengea.

    Akili zetu wanadamu huwa zinabadilika kama iliyo miili yetu, huwa tunakazana kubadili mambo ya nje badala ya kubadili mambo ya ndani ambayo ndiyo yapo ndani ya uwezo wetu.

    Kwa kuyakubali yale ya nje kama yalivyo, na kisha kubadili ndani ili kuweza kuendana na ya nje, ni njia ya kuchagua furaha kwenye maisha yako.

    Chukua hatua rafiki yangu tunapaswa kuwa na furaha kwa kuikubali dunia na kubadilika ili kuendana nayo.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.

  • Uongo unaokuzuiausianze.

    Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini licha ya watu wengi kujua wanachotaka, wengi wamekuwa hawaanzi kukifanyia kazi kwa sababu wanakubali uongo ambao wamekuwa wanajiambia kwa muda mrefu.

    Uongo huo ni kwamba bado hawajawa tayari. Ukweli unayopaswa kujua ni kwamba inapokuja kwenye kufanya chochote kikubwa na muhimu, hakuna wakati utajiona uko tayari.

    Hofu ya kuanza huwa inajificha kwenye utayari, ili uanze lazima uvuke hofu hiyo na uwe tayari kuanza hata kama bado hujawa tayari.

    Ukiyaangalia maisha yako, hatua zote ambazo umeweza kupiga, ulianza kabla hujawa tayari. Ulisukumwa kwa namna ambayo hukuwa na njia nyingine bali kuanza.

    Na ulipoanza, fursa nyingi zikafunguka mbele yako na ukaweza kufanya makubwa. Usikubali uongo kwamba hujawa tayari uwe kikwazo kwako kuanza. Anza kabla hujawa tayari na utaweza kufanya makubwa.

    Maendeleo yoyote kwa mtu, jamii na hata dunia kwa ujumla, huwa yanatokana na ujasiri wa mtu mmoja ambaye alikuwa tayari kuanza kabla hajawa tayari.

    Kwa mtu kuanza kabla hajawa tayari kuna faida kuu mbili.

    Faida ya kwanza ni kujenga ujasiri. Ujasiri ni matokeo ya vitendo na siyo maneno tu. Unapoanza kufanya kabla hata hujawa tayari, unapata ujasiri wa kuendelea kufanya.

    Faida ya pili ni mwendo. Kanuni ya mwendo inasema kilicho kwenye mwendo huendelea na mwendo na kilichosimama huendelea kusimama.

    Chukua hatua; kabla hujafanya maamuzi rafiki yangu tumeona umuhimu wa kuanza kabla hujawa tayari, tunapaswa kuanza kukifanya, na itakuwa rahisi kuendelea kukifanya, kuliko kungoja kuwa tayari ndio tuanze.

    Mwandishi wako,

    Maureen Kemei.

    kemeimaureen7@gmail.com.