Kwa Nini Hatupendi Kubadilika.

Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini yapo mambo ambayo tumekuwa tunajidandanya sana kwenye mafanikio, na haya yamekuwa yanachochea matatizo mengi tunayokutana nayo kwenye maisha.

Mambo yanayochangia tusibadilike ni kama yafuatayo;

Kwanza; tunajikadiria zaidi kwenye mchango wetu kwa mafanikio tunayofanya. Tunafikiria bila sisi mafanikio yasingepatikana, huku ni kujidanganya.

Pili ; tunachukua sifa ambazo hatustahili kuchukua, kazi wamefanya wengine lakini wewe kama kiongozi ndiye unayetaka upewe sifa.

Tatu; Huwa tunajiona tuna ujuzi WA juu kuliko wale wanaokuzunguka.

Nne; huwa tunapuuza muda na gharama ambazo tumeshapoteza kwenye miradi ambayo haizalishi.

Tano; kukuza matarajio ya mafanikio ya mradi, kuwa na mategemeo makubwa kuliko uhalisia.

Rafiki, uongo huu unatokana na mafanikio tuliyopata uko nyuma. Tunapopata mafanikio kidogo, huwa tunajiamini zaidi ya uhalisia.

Kujiamini huku kulikopitiliza ndiyo kunawaingiza wengi kwenye matatizo na kuwazuia kufanikiwa zaidi.

Mwandishi na rafiki yako,

Maure Kemei.

kemeimaureen7@gmail.com.

uamshobinafsi.com.

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment