Siri Ya Kuvuka Vikwazo.

Rafiki yangu mpendwa waliofika mbali waliamua kutokuogopa kushindwa.

Wao wanajaribu hata kama wanashindwa. Mafanikio ni ung’ang’anizi.

Mambo yakuzingazia ili kuvuka vikwazo.

  1. Kushindwa ni sehemu ya wastani. Baada ya hapana nyingi utapata ndio, hakuna kukata tamaa katika safari ya mafanikio. Wingi wa juhudi huleta kuua uoga wa kukataliwa.
  2. Kukataliwa hakumaanishi wewe ni tatizo bali ni bidhaa. Andika majibu ya mapingamizi ili utafute njia ya kuyavuka. Uliza maswali ili uweze kupata mapingamizi sahihi, kukataliwa ni kinga kukujenga uwe jasiri.
  3. Hakuna mafanikio bila kushindwa mara nyingi ni sehemu ya mchakato. Thomas Edison alishindwa mara nyingi kabla ya kupata mafanikio. Kushindwa siyo doa la aibu ni daraja la mafanikio.
  4. Kushindwa kunaonyesha ukweli wa juhudi zako. Mchakato uko ndani ya juhudi zetu na siyo matokeo. Frank Portugie alikuwa haweki kazi, alijitathmini na kuona ugumu na akaamua kufanyia kazi kwa kutaka matokeo. Ukiwa kinganganizi dunia inakupa kile unachokitaka. Fanya tathmini ujue ni juhudi ulizoweka ama ni uzembe uliokufikisha hapo, jiweke kitimoto.
  5. Ukiwa na hofu ya kushindwa utajifunga mwenyewe. Jaribu na kuwa kinganganizi hadi uweze kukubalika na wengine bisha mara nyingi au omba mara nyingi ili ukubalike.
  6. Kila hatua ya kushindwa inakusogeza kwenye kufanikiwa. Wingi wa majaribio unazalisha matokeo . Kukataliwa siyo wewe ni kile unachouza , jipime kwa juhudi zako.

Kile nimejifunza, kujaribu mara nyingi utaishia kwenye kupata matokeo. Kushindwa ni sehemu ya ushindi lakini ukiendelea kujaribu mara nyingi.

Rafiki yako,

Maureen Kemei

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment