Mara nyingi kile tunachohofia hata huwa hakitokei. Ni sisi tu binadamu huwa tunatengeneza mazingira ya hofu ambazo hata kiuhalisia hazipo.
Hofu huwa tunatengeneza akilini. Baada ya kuijaza hofu akilini mwili unapokea matokeo yake na hapo tunashindwa kuthubutu na kufanya kile tulichochagua kufanya.
Dawa ya hofu ni kukabiliana nalo mzima mzima, bila kujali nini kitatokea hata unachohofia saa zingine huwa hakitokei katika hali ya kawaida.
Twapaswa kutokuwa na hofu wowote, bali tuiachie asili ifanye kazi yake. Kama asili imepanga kutokea itatokea tu, na kama haijapanga kutokea haitatokea.
Hivyo usijali sana ni nini kitatokea baada ya kufanya kitu unachohofia sana, wewe fanya tu na matokeo yatakuja yenyewe.
Hatua ya kuchukua leo, usiwe na hofu, mara nyingi kile unachohofia huwa hakipo. Timiza wajibu wako acha kufikiria juu ya hofu.
Ukiwa mtu wa kujali hofu, hutaishi kwa amani, utakuwa na wasiwasi siku zote unapoamua kuchukua hatua fulani ya mafanikio.
Kuishi mara nyingi inahitaji ujasiri ili kuweza kukabiliana na hofu, ukiwa jasiri dunia itakuheshimu na kukupa unachohitaji, ukiwa mnyonge dunia itakuonea.
Mimi wako akujaliaye.
Maureen Kemei
Blog, kufikirichanya.wordpress.com