Rafiki, ni rahisi kuona waliofanikiwa kwenye kazi zao kama wana njia ya kupata mawazo bora kuliko wengine.
Unaweza kuona kama wao wana namna ya tofauti ya kupata mawazo ambayo wakiyafanyia kazi yanafanikiwa sana.
Ukweli ni kwamba watu wote huwa tunapata mawazo yanayofanana, mawazo mengi yako kwenye yale tunayofanya.
Kinachowatofautisha waliofanikiwa ni uwezo wao wa kuyachuja mawazo wanayopata na kujua yapi yana uwezo wa kuleta matokeo makubwa.
Wakati wasiofanikiwa wakihangaika na kila wazo wanalopata, wakijaribu mengi na wasipige hatua.
Wanaofanikiwa wanachuja mawazo hayo, wanaachana na mengi yasiyo sahihi na kufanyia kazi machache sahihi.
Hatua ya kuchukua ; rafiki, na wewe pia unaweza kujifunza na kuwa mchujaji bora wa mawazo unayopata ili kufanyia kazi yale yaliyo sahihi.
Unachohitaji rafiki yangu, ni kujua vizuri kile unachofanya na kuyasikiliza machale yako pia.
Akujaliaye sana.
Maureen Kemei
Blog:kufikirichanya.wordpress.com