Sifa pekee inayowatofautisha washindi na wale ambao wanashindwa ni uvumilivu na ung’ang’anizi.
Kama kweli mtu umekadiria au umeamua kutoka ndani yako kwamba lazima nifikie mafanikio makubwa. Utajitoa kweli kwenye kile unachokifanya na utapambania hadi ufanikishe jambo hilo.
Unapokutana na changamoto au kikwazo njiani, kwa vile uliamua kweli kupambana changamoto hizo haziwezi kukutoa. Lakini kama uliamua kwa kuangalia wengine wanafanya nini ukikutana na magumu yoyote lazima tu yatakutoa.
Unapoamua kuwa king’ang’anizi utapata upinzani mkubwa kutoka kwa familia yako, marafiki, na ata mwenzi wako, kwa maana wanaona unafanya kilicho tofauti na wao. Hivyo wanajaribu kukurudisha kwenye ukawaida katika hali kama hii uvumilivu na king’ang’anizi ni muhimu kuliko vingine vyote.
Unapaswa kufahamu kwamba vikwazo hivi ni vipimo tu, kama kweli umejitoa au upo tayari kutoa chochote kile ulichonacho ili kupata mafanikio unaotaka.
Tunajifunza leo kwamba kile tumeamua kufanya kwenye maisha ni vizuri tujitoe kweli, tung’ang’anie yale tunayofanya na hatimaye tutafikia kwenye uhuru wa maisha ambao ni mafanikio.
Imeandikwa na mwandishi na mshauri.
Maureen Kemei.
Blog, kufikirichanya.wordpress.com.
Ung’ang’anizi na uvumilivu asante Sana Maureem