Karibu, katika kujifunza zaidi kutoka kitabu cha 21 lessons for the 21st century kimeandikwa na Mwana historia Yuval Noah Harari.
Kwa kuwa tunaishi zama za taarifa ambapo maarifa yanapatikana kwa urahisi, watu wengi wamekuwa waifikiri wanajua sana. Watu wamekuwa wakiamini wanafikiri kwa kina na kufanya maamuzi sahihi.
Lakini tafiti zinaonesha huo siyo ukweli. Maamuzi mengi tunayofanya tunatumia kundi, kwa kuiga kile ambacho wengine wamefanya na kuamini ni sahihi na pia tunatumia hisia, tunatumia fikra zetu kwa kiasi kidogo.
Kuna vitu vingi sana vya kujua kiasi kwamba hakuna anayeweza kujua vyote, na kila siku vitu vipya vinagunduliwa. Hivyo badala ya kujidanganya kwamba tunajua sana na kufikiri tunafanya maamuzi kwa fikra zetu, ni vyema tukakubali udhaifu wetu ili tunapofanya maamuzi tujue hasa ni wapi tunaegemea.
Na zama tunazoishi sana ni hatari zaidi kwa sababu ujuzi wetu unazidi kupungua. Hii ni kwa sababu tunategemea zaidi wengine katika kufanya maamuzi. Watu wamekuwa wavivu wa kusoma vitabu na wanapenda kusikiliza wengine wanasema nini au wanafanya nini na wao ndiyo wafanye.
Ili kuondokana na hatari hii, lazima tuwe tayari kuweka muda na nguvu katika kuboresha ujuzi wetu na kuongeza maarifa tuliyonayo, hasa kwa yale maeneo muhimu kwetu.
Imeandikwa na mwanafunzi wa mafanikio, ushauri nasaha na uandishi.
Maureen Kemei
Blog, kufikirichanya.wordpress.com
Maisha yangu, uchaguzi wangu.