Rafiki yangu mpendwa kwenye hii tiba ya kuongeza kipato nimejifunza vitu vifuatavyo.
1. Ni lazima kutafuta namna yeyote ya kuongeza kipato ili kufikia uhuru wa kifedha.
2. Kutamani tu kuwa tajiri hakutakufikisha popote. Ila kutamani kupata vipande vitano vya dhahabu ni kitu kinachoeleweka na kinaweza fanyiwa kazi hadi kikatimizwa.
3. Lengo lako la kufikia utajiri iwe rahisi na kueleweka. itakuwa haina maana kama malengo yako ni mengi,hayaeleweki na yapo juu ya uwezo wako kuyatimiza.
4. Kadiri tunavyoongeza maarifa ndivyo tutakavyoongeza kipato chetu. Mtu atakaye jitahidi kuijua kazi yake vizuri atapata mafanikio zaidi.
5. Maisha ya mwanadamu hubadilika na kuwa bora kwa sababu ya watu wenye udadisi na wenye kutafuta ujuzi kwa faida ya wote.
6. Mtu anayejiheshimu anatakiwa kufanya mambo kama haya yafuatayo;
a). Anatakiwa kulipa madeni yake haraka iwezekanayo, hutakiwi kununua kitu usichoweza kumudu.
b).Anatakiwa kujali familia yake, hilo litafanya imheshimu na imuongelee vyema .
c).Anatakiwa kuacha wosia kwa maandishi ili siku akifa mali yake igawanywe kwa utaratibu.
d).Aanatakiwa kuwa na huruma kwa wagonjwa, wasiojiweza na wale waliopatwa na majanga. Awasaidie kulingana na uwezo wake.
e,).Anatakiwa kuwa mkarimu kwa wapendwa wake. kujifunza na kujizoeza kupata maarifa zaidi, kupata ujuzi zaidi na kujiendesha kwa heshima.
Rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com